Header Ads

Zaidi ya watu 60 wanahofiwa kufariki baada ya mashua iliyokuwa imebeba wahamiaji kupatikana karibu na Cape Verde

ZAIDI ya watu 60 wanahofiwa kufariki baada ya mashua iliyokuwa imebeba wahamiaji kupatikana karibu na Cape Verde huko Afrika Magharibi.

Watu 38 wakiwemo watoto waliokolewa huku picha zikiwaonesha wakisaidiwa kufika ufukweni, wengine kwenye machela katika kisiwa cha Sal.

Takribani wote waliokuwa kwenye mashua hiyo, ambayo ilikuwa baharini kwa zaidi ya mwezi mmoja, wanadhaniwa walikuwa wanatoka Senegal.

Maafisa wa Cape Verde wametoa wito wa kuchukuliwa hatua za kimataifa kuhusu uhamiaji ili kusaidia kuzuia hasara zaidi ya maisha.

Meli hiyo ilionekana kwa mara ya kwanza Jumatatu, polisi waliliambia shirika la habari la AFP.

Taarifa za awali zilidokeza kuwa boti hiyo ilikuwa imezama lakini baadaye ikafafanuliwa kuwa ilipatikana ikiyumba. Boti ya mbao ya mtindo wa pirogue ilionekana karibu kilomita 320 (maili 200) kutoka Sal, sehemu ya Cape Verde, na mashua ya uvuvi ya Uhispania, ambayo ilitahadharisha mamlaka, polisi walisema.

Walionusurika ni pamoja na watoto wanne wenye umri wa kati ya miaka 12 na 16, msemaji wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) alisema.

Boti hiyo iliondoka katika kijiji cha wavuvi cha Senegal cha Fasse Boye tarehe 10 Julai ikiwa na watu 101, wizara ya mambo ya nje ya Senegal ilisema Jumanne.

Moda Samb, afisa katika kijiji hicho, aliliambia shirika la habari la AFP karibu wote waliokuwa kwenye boti hiyo wamekulia katika jamii za hapo na kwamba baadhi ya familia za eneo hilo bado zinasubiri kusikia kama jamaa zao walikuwa miongoni mwa walionusurika.

Wizara hiyo ilisema inawasiliana na mamlaka nchini Cape Verde kupanga mpango wa kuwarejesha makwao raia wa Senegal.

Nchi nyingine za asili ya abiria hao zimeripotiwa kuwa ni pamoja na Sierra Leone na, mtu mmoja kutoka Guinea-Bissau.

Jose Moreira, afisa wa afya kuhusu Sal, alisema walionusurika walikuwa wakiimarika na walikuwa chini ya uangakizi wa wataalamu wa afya.

JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.chombohurumedia .blogspot.com ku-install App ya chombohurumedia,  bila ya kuingia website

Tweet@chombo huru media,Youtube@chombo huru media, Facebook@chombo huru media, Instagram @chombohuru­­_media

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.