Header Ads

YANGA SC YAWACHAPA ASAS 2-0 CHAMAZI


MABINGWA wa Tanzania, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, ASAS ya Djibouti katika mchezo wake wa kwanza wa Raundi ya Awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Mabao ya Yanga yamefungwa na wachezaji wake wa kigeni, kiungo wa Kimataifa wa Burkina Faso, Stephane Aziz Ki dakika ya 22 na mshambuliaji wa Kimataifa wa Zambia, Kennedy Musonda dakika ya 53.


Timu hizo zitarudiana Agosti 26 hapo hapo Chamazi Jijini Dar es Salaam na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla kati ya kati ya Otoho ya Kongo Brazzaville na El Mereikh ya Sudan kuwania tiketi ya makundi.

JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.chombohurumedia .blogspot.com ku-install App ya chombohurumedia,  bila ya kuingia website

Tweet@chombo huru media,Youtube@chombo huru media, Facebook@chombo huru media, Instagram @chombohuru­­_media

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.