OFISI YA RAIS, SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA YATOA MAFUNZO KWA MAMEYA WA MANISPAA NA WENYEVITI WA HALAMASHAURI na WAKURUGENZI WA SERIKALI ZA MITAA NCHINI.
Mwezeshaji wa Mafunzo kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo kwa Waheshimiwa Mameya, Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi wa Serikali za Mitaa nchini.
Mwezeshaji wa Mafunzo kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha , Dkt. Thadhei Kiwango, akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo kwa Waheshimiwa Mameya, Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi wa Serikali za Mitaa nchini.
Picha ya pamoja
washiriki wa mafunzo wakiwa na viongozi wa meza kuu katika uzinduzi wa mafunzo kwa Waheshimiwa Mameya, Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi wa
Serikali za Mitaa nchini.
Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Mhe. Nassor Mnambila ,Kamishna , Ofisi ya Rais, Tume ya
Utumishi wa Umma akimwakilisha Mhe. Jaji Mstaafu Sivangilwa S. Mwangesi katika uzinduzi wa mafunzo kwa Waheshimiwa Mameya, Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi wa
Serikali za Mitaa nchini.
OFISI ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma , imeendesha
mafunzo kwa Waheshimiwa Meya, Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi wa
Serikali za Mitaa nchini ikiwa ni juhudi za kuhakikisha viongozi hao
wanazingatia maadili ya umma na kufuata taratibu na kanuni za utumishi wa umma
kama inavyoelekezwa na Serikali.
Mafunzo hayo yamefunguliwa na Mhe. Nassor Mnambila ,Kamishna
, Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Umma akimwakilisha Mhe. Jaji Mstaafu
Sivangilwa S. Mwangesi.
Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Morena ,
Manispaa ya Morogoro , na yameendeshwa na Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya
Viongozi wa Umma kwa kushirikiana na Chuo Cha Uhasibu Arusha (IAA).
Akizungumza katika mafunzo
hayo Mhe. Mnambila, amesema kuwa mafunzo
hayo pia yatawajenga watumishi wa umma wakiwemo Mameya wa Manispaa na Wenyeviti
wa Halmashauri pamoja na Wakurugenzi wa Serikali za Mitaa ili waepukane na rushwa na matumizi mabaya ya
madaraka .
Mhe. Mnambila, amesema mafunzo hayo yanalenga
kuwajengea viongozi wa umma ujuzi wa kina kuhusu maadili katika uongozi,
utawala bora, matumizi ya fedha za umma, mifumo ya manunuzi, utoaji wa huduma
kwa wananchi, na jinsi ya kutambua na kuondoa migogoro ya kimaslahi.
“Kupitia mafunzo haya,
tunatarajia kuwa viongozi wetu watakuwa na uelewa mpana wa misingi ya utawala
bora na maadili katika utoaji wa huduma kwa umma, uongozi wenye maadili
huimarisha imani ya wananchi kwa Serikali na Taasisi zake , wananchi
wanapowaona viongozi wao mnatenda haki , uwazi na uadilifu ,huongeza
ushirikiano , utiifu wa sharia na mshikamano “ Amesema Mhe. Mnambila.
Hata hivyo, Mhe.
Mnambila, ametoa wito kwa viongozi wa
umma kuhakikisha wanafuata wajibu wao pamoja na kuyafanyia kazi mafunzo
wanayofundishwa.
Mwisho,amesema wanatarajia
kuona matokeo chanya yanayotokana na matunda ya mafunzo hayo.
Kwa upande wa Katibu Msaidizi
,Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini
na Mratibu wa Mafunzo, Gerald Mwaitebele, amesema mafunzo hayo yatasaidia kwa kiasi
kukubwa kuondoa mvutano kati ya madiwani
na wataalamu katika Halmashauri mbalimbali.
Aidha, Mwaitebele, amesema
mafunzo hayo yemefanyika ikiwa ni awamu ya pili na yote ni matokeo ya
ushirikiano kati ya taasisi mbili ikiwemo Ofisi ya Rais , Sekretarieti ya Maadili
ya Viongozi wa Umma na Chuo cha Uhasibu Arusha ambazo zimeingia makubaliano ya
kushirikiana katika kutoa mafunzo ya Maadili na Utawala bora kwa Viongozi wa
Umma, Kutoa ushauri kuhusu masuala yahusuyo Maadili pamoja na kufanya utafiti
kuhusu masuala yahusuyo Maadili.
Mwaitebele, amesema kuwa mafunzo hayo pia yatawajenga watumishi wa umma
ili waepukane na rushwa na matumizi mabaya ya madaraka pamoja na kuleta
mabadiliko chanya kwenye utendaji wa kila siku katika maeneo yao ya kazi ambayo
ni Mamlaka za Serikali za Mitaa .
Amesema kuwa yapo makundi
mbalimbali yatakayohusika na mafunzo hayo ikiwemo Wakurugenzi wa Utawala na
Rasilimali watu wa Wizara ,Taasisi na Mashirika ya Umma, Makatibu Tawala wa
Mikoa, Wakuu wa Taasisi za Umma na Wakurugenzi Wakuu wa Taasisi na Mashirika ya
Umma , Wajumbe wa Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma , Wakuu wa Idara na
Vitengo katika Wizara , Idara za Serikali , Taasisi za Umma , Mamlaka za Serikali
na Mashirika ya Umma.
“Tukaona ili
tuweze kuisaidia serikali tuwakumbushe wanatakiwa kufanya nini
tunawasisitiza kufanya kazi kwa pamoja wajue yanaeleweka lengo lao
ni nini dira yao ni nini, watumishi wa Umma Wanatakiwa kufanya kazi kwa pamoja
ili watende kwa kuwatimizia mahitaji wananchi,wakiwa hawana maeleano
itakuwa ngumu ndio maana tukaona tufanye mafunzo haya” Amesema Mwaitebele.
Kwa
upande wake, Mstahiki meya wa
halmashauri ya manispaa ya tabora Gullam
hussen Dewji amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo katika utendaji
kazi wao.
Dewji,amesema
kiongozi ni lazima afuate maadili ya
utendaji kazi kwani yeye anamilikiwa na umma hivyo ni lazima ahakikishe anavaa
vizuri pamoja na matendo yake yanakuwa mazuri.
“Tunaishukuru
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kutupa mafunzo haya, kwani ni
mafunzo muhimu na yanatengeneza ramani ya kujua viongozi wa uuma anatakiwa aishi
vipi na jamii inayomzunguka” Amesema Dewji.
















Post a Comment