Header Ads

DC KILAKALA AZINDUA MKOPO WA ASILIMIA 10 ROBO YA 3 NA 4 MWAKA 2024/2-25 NA KUWATAKA WANUFAIKA KUREJESHA KWA WAKATI.


MKUU wa Wilaya ya Morogoro,Mhe.Mussa Kilakala,  amewataka wanufaika wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Manispaa ya Morogoro  kwa ajili ya kuwawezesha kujikuza kiuchumi kuhakikisha wanairejesha mikopo hiyo kwa wakati ili iweze kuwasaidia wananchi wengine lakini pia kujiongezea kiwango cha ukopeshwaji ambapo katika robo ya tatu nay a nne kwa mwaka 2024/2025 Manispaa imetoa kiasi cha Tsh.681,776,700/=

Kauli hiyo ameitoa Julai 28-2025 katika uzinduzi wa utoaji wa mkopo wa asilimia 10 wa robo ya 3 na 4 kwa mwaka 2024/2025 kwenye Kituo cha zamani cha Stendi ya Daladala Mjini Kati.

Akizungumza na Wanufaika wa mikopo hiyo ambao ni wanawake,vijana na walemavu baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa utoaji wa  mikopo kutoka kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, amewasisitiza makundi yote kurejsha mikopo hiyo kwa wakati.

“Utoaji wa Mkopo huu wa asilimia 10  ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dkt.SamiaSuluhu Hassani juu ya kutenga fedha za mapato ya ndani ili kuwainua kiuchumi Vijana,Wanawake na Watu wenye ulemavu” Amesema DC Kilakala.

Aidha,DC Kilakala,amesema mikopo hiyo imekuwa na tija kubwa kwa kugusa makundi mbalimbali kama vile kundi la watu wenye ulemavu ambalo limeweza kuondokana na  utegemezi na sasa wanaweza kujihudumia wenyewe.

Katika hatua nyingine amewapongeza wanawake kwa  kuwa mstari wa mbele kwa kurejesha mikopo ya kwa wakati na kuwataka makundi mengine inayonufaika na mikopo hiyo kurejesha mikopo hiyo kwa wakati,kwa uwa imekuwa ni sehemu ya ajira na hivyo kupunguza uhalifu pamoja na utegemezi.

Hata hivyo,ameitaka Manispaa kuhakikisha wanavumbua walemavu kwani bado idadi ya walemavu wanaokopeshwa hairidhishi.

Pia,amewataka wananchi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29-2025 kwa ajili ya kuchagua viongozi watakaowaletea maendeleo.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Fikiri Juma, ameipongeza Menejimenti ya Manispaa chini ya Mkurugenzi  kwa usimamizi mzuri wa mikopo hiyo ya asilimia 10 na utaratibu mzuri wa utolewaji wa mikopo hiyo.

Fikiri, amempongeza Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya kwa ajili ya  kuleta maendeleo kwenye jamii,lakini pia amevipongeza vikundi vyote ambavyo vinarejesha  mikopo hii kwa wakati ,amewataka wanavikundi hao kujikita zaidi kwenye kufanya kazi  na kujitoa zaidi kwenye shughuli za maendeleo  kutoka na mikopo hiyo.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro,Emmanuel Mkongo, amesema mwaka 2024/2025 Manispaa ilitenga Tsh.1,305,455,455,433.10 na kwa mwaka 2025/2026 imetenga Tsh.1,351,135,667.00 kutoka kwenye asilimia 10 ya mapato ya ndani.

Mkongo amesema, jumla ya vikundi 74 vikiwemo vikundi 49 wanawake, 17 Vijana na 08 watu wenye ulemavu vilipatiwa mkopo ambapo wanawake walipatiwa shilingi 421,509,000, Vijana shilingi 231,836,000 na Watu wenye ulemavu shilingi 28,440z,700.

Aidha, Mkongo, amewahakikishia wanavikundi kuwa pesa za mikopo zipo hivyo vikundi viendele kujitokeza ili kupata mikopo hiyo na kutumia kujikuza kuichumi na sio kuitumia kwa njia tofauti.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Manispaa ya Morogoro,Khadija Mbwana amewataka wanufaika wa mikopo hii isiyo riba kuitumia vizuri ili kuinua maisha yao .

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.