Header Ads

Mkuu wa Wilaya Morogoro atoa siku 4 kwa Manispaa kuwawajibisha Watendaji watakao kutwa na taka taka katika vipande vyao vya mito na mifereji.



MKUU wa Wilaya ya Manispaa ya Morogoro, Mhe Regina Chonjo, ametoa tamko kwa Manispaa na akitaka kupata taarifa ndani ya siku 4 kwa Watendaji wa Kata kuhakikisha  taka taka zote zilizopo katika mito na mifereji zinaondoka.

Hayo ameyasema hivi karibuni kwenye Viwanja vya Hospitali ya Rufaa Morogoro kufuatia malalmiko ya Wananchi juu ya kuwepo kwa taka taka kwenye mito na mifereji, jambo linalosababisha mito kuziba na kuleta maafa kwa Wananchi.

Aidha, DC Chonjo, amesema kuwa taka taka zikidi katika mito husababisha mafuriko katika maeneo wanayoishi Wananchi wakati wa mvua, hivyo kila mtendaji awajibike kuhakikisha mito hiyo inakuwa salama na kila Mwananchi awe mlinzi wa mwenzake.

DC amesema ,kumekuwa na malalamiko katika Mto Kikundi kwenda Mto Mwembe Songo, Wananchi wakilalamika kuwepo na mrundikiano wa taka taka na  kusabisha mafuriko  mvua ikinyesha, hivyo katika kuona kero hiyo inataturiwa amemuagiza Mhandisi wa Manispaa, Juma Gwisi, kuhakikisha wanaweka bajeti ya kufua Mito hiyo  na kuona jinsi ya kusafisha ili wananchi wasipate madhara.

Kwa upande wa Mhandisi wa Manispaa ya Morogoro, Juma Gwisu, amesema Manispaa imetenga Bajeti katika mwaka wa fedha mwaka 2019/2020 , kwa ajili ya kufanya matengenezo ya mifereiji pamoja na mito ili kuzuia mafuriko na kuweka mipango mikakati ya kusimamia usafi katika mifereji ya mitop hiyo.

"Ni kweli malalamiko hayo yapo, lakini juhudi tunazo zifanya kila ifikapo kipindi cha mvua  Manispaa tunafua mito hiyo, ili kuepusha maji kujaa na kufikia katika nyumba za watu, hivyo katika mwaka huu tumeanza kupata fedha na tumejenga kipande cha Km 2.4 kutoka Mto Mkundi na sehemu iliyobakia kadri bajeti itakavyopatikana, tutaendelea na ujenzi huo" Amesema Gwisu

Aidha, amesema baadhi ya maeneo yenye uchafu yanasababishwa na wakazi wenyewe, kwani nyumba zinajengwa karibu na mito na wakazi waishio maeneo hayo wanafanya mito hiyo kama dampo la kutupia taka taka.

Amewataka Wananchi washirikiane na Manispaa ili kuepusha utupaji taka taka hovyo katika mito hiyo na kuepuka madhara yanayowakumba Wananchi kipindi mvua inaponyesha.



No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.