Header Ads

WAMACHINGA MOROGORO WAIPONGEZA HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOROGORO KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO.




Mkurugenzi Manispaa Morogoro, Sheilla Lukuba, akipokea Cheti cha Pongezi Ofisni kwake  kutoka kwa Mwenyekiti wa Wamachinga Wilaya ya Morogoro,  Ndug. Faustine Alimas. 

 UONGOZI wa Wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu Machinga wa Halmashauri ya  Manispaa ya Morogoro,  wameipongeza  Halmashauri ya  Manispaa Morogoro kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo ikiwamo ya kimkakati.

Akizungumza kwa niaba ya Wamachinga wa Morogoro, Mwenyekiti wa Wamachinga Manispaa ya Morogoro, Ndug Faustine Alimas , amesema Manispaa inafnya kazi kubwa katika kusimamia miradi ya maendeleo na ina  stahili kupongezwa.

Amesema katika kipindi hiki cha karibuni, wameshuhudia mabadiliko makubwa sana hususani katika miradi inayotekelezwa katika Manispaa hiyo ikiwamo miradi mikubwa ya kimkakati kama vile mradi wa Soko Kuu la kisasa lililopo Kata ya Mji Mkuu pamoja na Mradi wa Stendi Mpya.

Amesema kuwepo na miradi mikubwa ndani ya Manispaa kutasaidia kuingizia Manispaa pato la ndani na kuacha kutegemea fedha za Ruzuku kutoka Serikali kuu.

Pia wamempongeza Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, kwa kuwa karibu nao na kuwashirikisha  kwa kila jambo kitu ambacho kinawajengea faraja Wafanyabiashara na kuona Serikali inawaunga mkono kama alivyotamka Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kuwataka Wamachinga kufanya biashara zao bila ya kubugudhiwa.

"Mkuu wa Wilaya Mama yangu Mhe. Regina Chonjo, tunakushukuru sana pamoja na Uongozi wako wa Wilaya, umekuwa msaada mkubwa sana kwa upande wetu, umesimama mstari wa mbele kuhakikisha maslahi ya Wamachinga unayasimia kikamilifu, pia tumeona Manispaa inabadilika , miradi mikubwa mnayoitekeleza kwakweli inatupa faraja sana sisi wana Morogoro, kwani tunaamini baada ya kukamilika miradi hii Manispaa tutakuwa tuna vyanzo vizuri vya kukusanya mapato yetu ya ndani na kutengeneza miradi mingine kwa lengo la kuwahudumia Wananchi, nichukue nafasi hii kusema tunaomba usituchoke mama yetu tunapopatwa na changamoto zidisha nguvu zako za kutukwamua" Amesema Almas.

Aidha, amechukua nafasi hiyo kwa kumpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, huku akisema wapo tayari kumpa ushirikiano wakutosha kwani lengo lao sio kubaki nyuma ni kusonga mbele.

"'"Tunapenda kumkaribisha Mkurugenzi katika Manispaa yetu, tunamhakikishia tutakuwa nae bega kwa bega na taarifa zozote atakazo zihitaji tutampatia lengo ni kuijenga Manispaa yetu isonge mbele na wamachinga wasonge mbele, tunamuomba kwa muda wake tuweze kuonana naye sisi viongozi na tuanze kumpatia maelezo juu ya Chama chetu, mikakati , mafanikio pamoja na changamoto ziazotukabili" ameongeza Almas

Hata hivyo, amewaomba Wafanyabisahara wenzake kuwa ruhusa ya kibali cha wao kupanga biashara zao barbarani sio wakiuke shereia ,wanatakiwa kuzingatia sheria na kuhakikisha mara baada ya kufanya biashara zao wasogeze meza pembeni ili kuruhusu maeneo hayo yaweze kutumika kwa matumizi mengine.

Pia wamemshukuru Mhe. Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kuwapatia kibali cha kufanya biashara zao pembezoni mwa barabara na kando kando ya mitaa kwani awali waliishi maisha ya kutanga tanga ya  kunyang'anywa bidhaa zao lakini Mhe. Rais ameliona hilo na kuwaondoa  kwenye mateso.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.