Header Ads

RC SHIGELA ARIDHISHWA NA UJENZI WA MADARASA YA UVIKO 19 SHULE YA SEKONDARI KINGOLWIRA.

 






MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Martine Shigela, ameridhishwa na ubora wa ujenzi wa madarasa 4 yaliyojengwa kupitia mpango wa UVIKO 19 katika Shule ya Sekondari Kingolwira Manispaa ya Morogoro.

Kauli hiyo ameitoa Juni 08/2022 katika ziara yake ya kukagua ujenzi huo alipopita akiwa na Mkutano wa Kusikiliza na Kutatua kero za Wananchi wa Kata ya Kingolwira.

RC Shigela, amesema Serikali imeendelea kutekeleza kwa mafanikio makubwa Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mpambano dhidi ya Ugonjwa wa Visrusi vya Korona (UVIKO 19) wenye thamani ya Shilingi Trioni 1.3 kwa kuimarisha upatikanaji wa huduma za jamii ambapo kwa Mkoa wa Morogoro fedha hizo zimeweza kunufainisha katika Sekta ya elimu na Afya.

Aidha, RC Shigela, ameupongeza  uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa
kusimamia vilivyo hadi kukamilisha kwa wakati miradi hiyo ya ujenzi wa
madarasa ya fedha za UVIKO 19.

“ Nimeona hapa mmeenda vizuri madarasa yana ubora, pia niwaopongeze kusimamia miradi hii kikamilifu Rais wetu Samia Suluhu ametuletea Bilioni 1 na laki 7 na nimeona madarasa 86 mmeyakamilisha vizuri na watoto wetu wanasoma kwa nafasi na waalimu pia wanafundisha kwa ufanisi mkubwa, kikubwa Wanafunzi wasome kwa bidii na waalimu wafundishe kwa bidii” Amesema RC Shigela.

Mwisho, RC Shigela, amewaagiza wakurugenzi kuhakikisha kwamba wanatenga fedha kupitia mapato yao ya ndani  kwa kushirikiana na nguvu za wananchi kuelekeza nguvu zao katika ujenzi wa matundu ya Vyoo pamoja na ujenzi wa nyumba za Waalimu ili waalimu waishi jirani shule.

Kwa kipindi cha mwaka mmoja wa mheshimiwa Rais samia Suluhu Hassan Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro idara ya Elimu Sekondari wamepokea kiasi cha Tsh, 1,720,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 86 vya madarasa.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.