Header Ads

BUTABILE AWATAKA VIONGOZI KUZINGATIA MAADILI NA UADILIFU KATIKA KUTOA HUDUMA KWA WANANCHI

 

VIONGOZI wa Mitaa   na wadau mbalimbali watakiwa kuishi kwa maadili na uadilifu ili kujenga nguzo bora yenye  kuleta tija katika kukuza na kuchochea maendeleo.

Hayo yamebainishwa na Diwani wa Kata ya Mafiga Mhe. Thomas Butabile, akiendelea na ziara yake katika Mtaa wa Misufini ambapo amesema  kufuata maadili siyo matukio bali inapaswa kufanywa kwa maisha ya kila siku .

" Mfano mtu anakunywa hakatazwi lakini  unakuta mtu anakunywa mpaka anashindana kuzungusha laundi ukiulizwa unasema nalinda kura au naamasisha wananchi huku ndipo wapo wengi tuache tabia hizo na tujidhibiti na kufanya Kazi ipasavyo kama anavyofanya Rais wetu Dkt. Samia Suluhu hassan  ili kuleta maendeleo kwa kasi"Amesema Butabile.

 Butabile amewataka wananchi wasisite kutoa taarifa ili kupatiwa haki zao kwa kuwa wao  ndiyo wamebeba dhamana ya wananchi.

Naye Afisa wa Maadili mwandamizi Mkoa wa Morogoro,Jackline Msumba,   amesema  madhara ambayo yanawezwa kuletwa na kiongozi asiyekuwa na maadali ni makubwa hivyo yawapasa kutambua uongozi ni dhamana ya kuhakikisha unatekeleza majukumu uliopatiwa kikamilifu.

Msumba, amewataka Wananchi wa kata ya Mafiga  kutoa taarifa mapema endapo kiongozi hatafuata maadili ya Uongozi wake.

"kazi ya Viongozi ni  kuhakikisha viongozi wanawatumikia wananchi lakini kwa  kufuata kanuni na siyo kuvunja sheria" Amesema Msumba.

Ziara ya Mhe. Butabile imeendelea leo Novemba 07/2023 katika Mtaa wa Polisi  akimabatana na wataalamu mbalimbali kutoka Ofisi za Umma pamoja  na Ofisi ya Kata.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.