Header Ads

KAMATI NDOGO YA AFYA MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KERO ZA VITUO VYA AFYA ZITATULIWE KWA WAKATI.


KAMATI ndogo ya afya Manispaa ya Morogoro ikiongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Rashid Matesa, imefanya ziara ya kukagua miradi ya afya  katika Manispaa hiyo na kuagiza Uongozi wa Manispaa kutatua haraka changamoto zinazojitokeza katika Vituo vya Afya.

Ziara hiyo imefanyika Julai 12/2023 huku msisitizo wa kamati hiyo ni kukamilika kwa wakati miradi ya afya ili ianze kutoa huduma.

Aidha, Kamati hiyo pia imetoa pongezi kwa Mkurugenzi na Wataalamu katika  uendeshaji wa miradi kwa kuzingatia viwango ikiwemo ubora wa majengo pamoja na kasi ya uendeshaji.

Pia, hiyo imesisitiza kuwa  katika changamoto zilizopatikana kwenye baadhi ya miradi kutiliwa mkazo kuhakikisha zinafanyiwa kazi ikiwa ni moja ya kazi ya kutimiza majukumu ya kamati.

Mwisho, Kamati hiyo, imemuagiza Mganga Mkuu wa Manispaa  kuhakikisha katika Vituo vya afya na Zahanati zinapohitaji wauguzi basi wawapeleke kwa haraka ili huduma ziendelee kutolewa.

JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.chombohurumedia .blogspot.com ku-install App ya chombohurumedia,  bila ya kuingia website

Tweet@chombo huru media,Youtube@chombo huru media, Facebook@chombo huru media, Instagram @chombohuru­­_media

SUBSCRIBE YOUTUBE CHANNEL: chombo huru media.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.