Header Ads

Mkuu wa Wilaya, mkurugenzi Manispaa ya Morogoro wawakumbuka Watoto yatima na Wazee wasiojiweza kuelekea kukaribisha Mwaka mpya.



Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro , Sheilla Lukuba wamefanya matembezi ya  kuwakumbuka Jamii kwa kutekeleza utoaji wa zawadi za Vyakula na Vinywaji kwa Makao ya kulelea watoto yatima cha MGOLOLE  kilichopo wilaya ya Morogoro.

Akikabidhi vitu hivyo vyenye thamani ya Shilingi Milioni 1,kwa upande wa Mkuu wa Wilaya, Mhe. Regina Chonjo, amesema kuwa Ofisi yake ya Wilaya na Manispaa kwa ujumla iko pamoja nao na itaendelea kushirikiana nao kwa mazuri na changamoto yeyote katika makao hayo na wasisite  kutoa taarifa pale wanapokuwa na tatizo lolote.
“Nimmefurahishwa sana na huduma mnazowapatia watoto wetu, kwakweli mnastahili pongezi kubwa ni wachache wenye moyo kama wenu wa kuwasaidiahawa watoto, msikkate tamaa endeleeni na malezi bora mwenyezi mungu atawabariki sana chukueni hiki kidogo tulichowaletea ikiwa ni sehemu yetu ya kusherekea mwaka mpya na watoto wetu wajisikie huru na Amani badala ya kuwa wapweke”Amesema DC Chonjo.
Pia amempongeza mlezi wa kituo hicho, Sister Palagia Maria, kwa kuwa na malezi mazuri kwa watoto hao wanaoletwa kwenye Makao hayo wakiwa katika mazingira hatarishi.
Aidha Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amesema kuwa huo ni mwendelezo wa ahadi zilizotolewa na Mkuu wa Wilaya kwa kushrikiana vyema na Uongozi wa Manispaa ya Morogoro huku akisema kuwa  tayari baadhi ya ahadi zimekwisha tekelezwa na zawadi nyingine kutoka kwa wahisani hivyo amemtaka mlezi wa Makao hayo waendelee na moyo wa kuwasaidia  watoto hao hadi pale watakapo pata mwangaza wa maisha yao.
“Watoto niwaombe msome sana mkizingatia hakuna urithi Zaidi ya elimu, Serikali ya awamu ya tano chini ya Mhe. Rais Dkt. John Magufuli imewekka mpango wa elimu bila malipo msome sana ili nayi baadae muweze kuwa na masiha mazuri na kuendesha familia zenu” Amesema Sheilla.

Naye, Mlezi wa Makao hayo, Sister Palagia Maria, amemshukuru Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi ikiwamo Ustawi wa Jamii kwa kuwa karibu nao huku akiwataka wasikate tamaa kwani wao wanategemea pia misaada kutoka kwa wahisani.
Mbali na kutoa chakula pamoja na Vinywaji katika Makao ya Mgolole, Mkurugenzi Sheilla amepata nafasi ya kutembele kituo cha kulelea Wazee wasiojiweza cha Funga Funga kilichopo  Manispaa ya Morogoro na kutoa zawadi ya TV Flat Screen na king’amuzi cha Star Times vyenye thamani ya Shilingi Laki 7.
Amesema lengo la kutoa Tv hiyo ni kuwafanya Wazee hao waweze kuangalia mambo mbali mbali ya maendeleo yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya tano chini ya Mhe. Rais Dkt. John Magufuli.
Kwa upande wake Afisa Mfawidhi Kituo cha Funga Funga, Bi Yolanda Komba,amemshukuru Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi na Idaraya Ustawi wa Jamii kwa kuwa karibu na kuwasaidia katika huduma mbali mabli ikiwamo kuwapatia msaada na kuwajali wazee  hao wenye mahitaji muhimu hivyo anamtakia kazi njema katika kutekeleza majukumu yake na kuanza mwaka mpya kwa mafanikio zaidi.
Naye Mwenyekiti wa Wazee hao, Mzee Joseph Kaniki, ameushukuru Uongozi wa Manispaa ya Morogoro kwa kutekeleza akile walichokiomba huku akizidi kumuombea Mhe. Rais Magufuli afya njema ili aweze kuiongoza vyema Tanzana katika kufikia maendeleo hususani uchumi wa Kati na Viwanda.












No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.