Header Ads

MKURUGENZI Manispaa Morogoro awataka Watumishi wa Kike kulitumia Sanduku la Maoni kukomesha unyanyasaji wa Kijinsia kazini..



MKURUGENZI wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amesema   kuwepo kwa  Sanduku la maoni kutawafanya Watumishi Serikalini na Sekta binafsi kuwa huru  kutoa Maoni dhidi ya vitendo viovu. 

Hayo ameyasema leo Desemba 3, 2019, wakati Jamii ikiwa ndani ya maadhimisho ya  Siku 16 za   kupinga Ukatili wa Jinsia Duniani.

 Aidha amesema kuwa, dhumuni la  Sanduku hilo ni kuwafanya Watumishi   kutoa Taarifa ya matukio ya unyanyasaji wa  kijinsia . 

Katika upande mwengine, amesema matendo ya ukatili wa jinsia  yanafanywa sana na wanaume hivyo uwepo  kwa Sanduku la maoni  litawafanya Watumishi wakike  kuwa huru huku akisema kwamba wale wote  watakaobainika kuwa na tabia hiyo watachukuliwa hatua Kali za kisheria  .

 Amesema kitendo cha unyanyasaji Wa kijinsia ni kinyume na Sharia ya ajira na mahusiano kazi Namba 6 ya mwaka 2004.

" Najua Sanduku hili lipo hapa lakini katika siku hizi za Kupinga Ukatili wa Jinsia tuanze kutambua umuhimu wa Sanduku hilo , tumelifunga hapa Ofisini  kwa kuzingatia eneo litakalofikika kwa watu wote na ndugu zetu wenye ulemavu wapate fursa ya kutoa maoni yao, tunamshukuru Mkuu wetu wa Wilaya, Mhe. Regina Chonjo  kwa kuwa karibu na Wanawake hii inaonesha ni kwa jinsi gani anatekeleza vyema Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuelekea Uchumi Wa kati na Tanzania ya Viwanda kwa kuwawezesha Wanawake , Wakina mama, Vijana na Walemavu" Amesema  Sheila.

 Amesema kuwa miongoni mwa Vitendo wanavyokutana navyo Watumishi Wa  kike  ni pamoja na Rushwa ya ngono , udharirishaji Wa kijinsia na kudharaurika.

Ikumbukwe kwamba agizo hilo lilitolewa kwa Halmashauri  pamoja na Manispaa  zote kwa makatibu Wa Wilaya kufanikisha kuwepo kwa Sanduku la Maoni ambapo Manispaa ya Morogoro ilianza  mapema kumkomboa Mwanamke.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.