Header Ads

Manispaa ya Morogoro yageuka chuo cha mafunzo miradi ya Kimkakati, Meya aeleza jinsi wanavyoweza kusimamia mapato.

Watumishi na Madiwani wa Manispaa ya Morogoro wakiongozwa na Mhe. Meya Kihanga wakiwa katika picha na Watumishi pamoja na Madiwani wa Halmshauri ya Mji Bariadi wakati wa ziara ya H/Mashauri Bariadi kufanya ziara ya kikazi ya Kujifunza ukusanyaji wa mapato Desemba 23,2019.

HALMSHAURI ya Manispaa ya Morogoro, imezidi kuchanja mbuga katika utekelezaji wa Miradi ya Kimkakati hii ni kufuatia wiki mbili hivi karibuni kutembelewa na Halmshauri  mbili tofauti kwa wakati mmoja katika kujifunza namna ya ukusanyaji wa mapato na njia bora ya usimamizi wa miradi ya Kimaendeleo hususani miradi ya Kimkakati.


Akizungumza na Waandishi wa Habari, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga,amesema kuwa Manispaa ya Morogoro ina miradi mikubwa  mitatu ya kimkakati ukianzia Stendi ya Msamvu  ambayo imeshaanza kufanya kazi, lakini pia  Soko Kuu la kisasa ambalo linaendelea kujengwa na Stendi ya daladala.

Amesema kuwa katika Jengo la Stendi ya Msamvu ambacho ni kituo bora cha Mabasi Afrika Mashariki kilichojengwa na Kampuni ya Msamvu Property Ltd , waliingia ubia na  LAPF  kwahiyo fedha zinazopatikana zinaingia kwenye mfuko huo, na pia faida inayopatikana wanagawana na  tangia stendi hiyo  ianze  kazi wameshagawana faida  mara moja.

Aidha, amesema kuwa katika  faida waliiyogawana walifanikiwa kutenga jumla ya Shilingi Milioni 140 , hivyo katika mgawanyo huo Manispaa waliweza kupata Shilingi Milioni 40 kwa kuwa waliwekeza asilimia 40% na LAPF walipata milioni 100 kwa uwekezaji wa asilimia 60 na zaidi.

Amesema kuwa miradi mengine ikikamilika wataweza kukusanya mapato makubwa ya vyanzo vya ndani kutoka shilingi Bilioni 6.7 za sasa hadi kufikia Bilioni 10 na zaidi.

""Mradi huu ni mkubwa lakini tuliingia ubia na LAPF  kwa asilimia ,  wenzetu walivyowekeza zaidi wao wana asilimia 60 na sisi  Manispaa tuna asilimia 40 lakini asilimia hii 40 ya kwetu ilipungua kutokana na wenzetu waliwekeza zaidi, kwahiyo katika kugawana wao walipata milioni 100 na sisi tukapata milioni 40, lakini bado fedha zipo benki kwa ajili ya kupata faida kubwa , kwahiyo miradi hii itatuongezea mapato makubwa sana katika Manispaa,mradi huu mhe. Rais alishasema urudi ndani ya manispaa inaweza kututoa kutoka kwenye bilioni 6.7 hadi kwenye bilioni 10 na kadhaa na hiyo inawezekana  tunatarajia soko letu litaisha Mwezi 2 , Mwaka 2020  na soko hilo ni fedha za kimkakati hatudaiwi na mtu hivyo tutaanza kukusanya wenyewe na mapato ya Manispaa yataongezeka hata hivyo stendi ya daladala nayo itakamilika mwezi wa 5 mwaka 2020 na fedha hizo pia ni za kimkakati" Amesema Mhe. Kihanga  

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Bariadi Mkoa wa Simiyu, Mhe. Robert Mgata, ameipongeza Manispaa ya Morogoro kwa usimamizi mzuri wa makusanyo ya kodi na njia bora ya kuendesha miradi.

Amesema lengo la kuja Morogoro, namna bora ya ukusanyaji wa mapato pamoja na usimamizi wa miradi , hivyo matumaini yake ni mara baada ya kurudi Bariadi wataenda  kuweka njia bora ya usimamizi wa miaradi ili kuongeza ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri yao.

Aidha, amesema Halmshauri ya Mji Bariadi tayari imeaanza ujenzi wa Stendi Mpya ya Kisasa na mpaka sasa ujenzi huo upo asilimia 95 kukamilika.

Amesema kuwa walichokipata  na elimu pana ya ukusanyaji wa kodi wanaamini kabisa watapiga hatua na pengine kuwa moja ya Stendi bora kabisa nchini Tanzania katika suala zima la ukusanyaji wa mapato na usimamizi wa wa kutawala.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.