Header Ads

WAITARA ARIDHISHWA NA USAFI MANISPAA YA MOROGORO, ATAKA KASI IONGEZWE KATIKA UPATIKANAJI WA DAMPO LA KISASA

         

Afisa Dampo, Alex Roman (wapili kutoka kulia) akisikiliza kwa makini maelekezo ya Mhe. Waiata ya kuboresha dampo.(wapili kushoto), Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga. (katikati), Mkurugenzi Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba.

           

Mhe. Diwani wa Kata ya Mafisa, Mhe. Joelly Kisome (kushoto), akizungumza na Mhe. Waitara mara baada ya kuwasili Dampo la taka Manispaa ya Morogoro.

               

              


             

Afisa Mazingira Mkoa wa Morogoro, Venance Soza Segere,  akisoma taarifa ya Mazingira Mkoa wa Morogoro.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Bakari Msulwa, akitoa taarifa ya hali ya mazingira katika Wilaya ya Marogoro.

Afisa Mazingira Manispaa ya Morogoro, Samweli Subi, akisoma taarifa ya Mazingira Manispaa ya Morogoro.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mazingira Manispaa ya Morogoro na Diwani wa Kata ya Kihonda, Mhe. Hamisi Kilongo, akizungumza juu ya mipango ya kamati hiyo katika utekelezaji wa mazingira na Usafi wa Mji.
           

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mwita Waitara, ameipongeza Manispaa ya Morogoro kwa mipango mizuri na usimamizi mzuri wa usafi huku akitaka nguvu iongezwe katika ufuatiliaji wa Dampo la Kisasa.

Kauli hiyo, ameitoa leo wakati wa ziara ya ukaguzi wa Dampo la taka Manispaa ya Morogoro lililopo Kata ya Mafisa.

''Nimefurahishwa  sana na hali ya hatua za kuanza kutekeleza  ujenzi wa Dampo la Kisasa, mmeniambia tayari andiko lipo na mshaliwasilisha kazi yangu mimi ni kusukuma ili hizo fedha zitoke, lakini niwaombe Dampo la kisasa lizingatie miundombinu yote, lisiwe kama hili la kienyeji hapa tushakosea kikubwa kuhakikihsa wakati tunajiandaa na ujenzi wa Dampo Jipya , hili tulilo nalo tuliwekee mazingira rafiki taka zisibaki nje, hapa kuna taka zipo ambazo zinazalisha sumu, haya maji yakitiririka yanawafikia wananchi na ni hatari kwa afya, 

Aidha, amesema sio jambo baya Manispaa ikatoka ziara kwa ajili ya mafunzo ya kuona wenzao walivyojipanga katika ujenzi wa Madapo lakini hata katika usafishaji wa Mji .

Mhe. Mwita, amesema kutohudumia  dampo hilo ipasavyo kunapelekea  uchafuzi wa Mazingira  harufu mbaya,  na maji yenye sumu kali  na kuhatarisha afya ya wakazi wa maeneo jirani viumbe hai na mzingira kwa ujumla.

Nawapongeza sana kwa hatua hii ya kuanza kubuni mchakato wa  utekelezaji wa mradi wa Dampo jipya, lakini kwa hatua nzuri za  usimamizi mzuri wa usafi, kama mlivyosema mataka kwenda jiji, hatuwezi kuwa Jiji wakati bado kuna taka zinazagaa mitaani, jipangeni vizuri, mmesema mshawasilisha taarifa na andiko la mradi wenu, tutasukuma kuona hizo fedha zinatoka ilia ujenzi uanze, kisha ujenzi huo uzingatie miundombinu mizuri ya Dampo, lakini kikubwa zaidi endeleeni kutoa elinmu kwa wananchio wenu jinsi ya kutengeanisha taka nyumbani ili waone taka ni dili na sio uchafu mara baada ya kuanzisha kiwanda chenu cha uchakataji wa takataka" Amesema Mhe. Waitara.

Katika ziara hiyo ameitaka Halmashauri kuwa na mikakati mizuri ya kusimamia usafi ikiwamo kuwa na mbinu bora za kufanya kila mmoja kuona jukumu la usafi ni lake na kuwa na sheria ambazo zitatekelezwa kwa asilimia mioa moja katika usafi ikiwamo na tozo za usafi na faini kwa wale waharibifu wa mazingira.



 “ Hakuna kitu nisichopenda katika utendaji wangu kama kuona taasisi za serikali zikiwa za kwanza katika suala zima la uchafuzi wa mazingira, hakikisheni mnakwepa lawama za wananchi, maji yakiwa machafu hapa yanatengeneza sumu kutokana na takataka na kuelekea katika  makazi ya wananchi , hakikisheni kama yapo tengenezeni mifereji ya maji ya mvua, na maji ya sumu yaende katika mkondo sahihi wa maji hatarishi na bila kusahau kuruhsu maji hayo baada ya kujiridhisha na vipimo vinavyotakiwa" Ameongeza Mhe. Waitara.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Bakari Msulwa, amesema Wilaya ya Morogoro inakabiliwa na changamoto nyingi za kimazingira lakini wapo tayari sasa kuanza kutekeleza maagizo hivyo watajipanga na timu ya wataalamu kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkoa na NEMC ili kuona changamoto hizo zinafanyiwa kazi.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, amesema wapo katika hatua za kuhakikisha kwamba Kamati zote za Mazingira zinafanya kazi ipasavyo ili kuondokana na tatizo hilo.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba,amesema Manispaa ya Morogoro imetengea bajeti ya shilingi milioni 300 kwa ajili ya ununuzi wa  gari la taka ili kuongeza nguvu.

Awali akitoa taarifa ya hali ya mazingira  na usimamizi wa taka katika Dampo, hilo, Afisa  Dampo, Alex Roman, , amemueleza Mhe. Waitara kuwa, Dampo hilo linakabiliana na changamoto mbali mbali ikiwa ni pamoja dampo  kutokuwa la kisasa , idadi ya watu wanaongezeka pamoja na uzalishaji wa taka ktika Kiwanda cha Mpunga.

Romani, amesema, kwa siku Dampo hilo linapokea tani 180 hadi 200 za taka zinazozalishwa na kuingia katika dampo hilo.

Amesema katka kuhakikisha changamoto hiyo inakwisha, Manispaa ya Morogoro imeandaa eneo Kiega lenye zaidi ya hekari 1000 ili kujenga Dampo la kisasa.
""Changamoto ipo kubwa, kwahiyo eneo hili halikuwa kwa ajili ya dampo bali ni eneo ambalo lilitengwa kwa ajili ya Viwanda, hivyo tumeshaanda eneo Kiegeya lenye zaidi ya hekari 1000 ambalo tunatarajia eneo hilo kujenga Dampo la kisasa litakalo kuwa na miundombinu yote" Amesema Romani.




No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.