Header Ads

MTENDAJI KILAKALA ATAKA MAPAMBANO DHIDI YA UDUMAVU


Wananchi wa Kata ya Kilakala wakipata  lishe.
Mtendaji wa Kata ya Kilakala, Amina Saidi, akipika uji kwa ajili ya kuwagawia watoto .

MTENDAJI wa Kata ya Kilakala, Amina Saidi, ametaka   wadau wa lishe   kupambana  kutokomeza udumavu ndani ya Manispaa ya Morogoro hususani wakazi wa Kata ya Kilakala  ili  kuwa na jamii  bora  isiyo na udumavu .

Kauli hiyo imetolewa Januari 24/2021 katika maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe Kata ya Kilakala iliyofanyika katika eneo la Soko la Kilakala.

Akizungumza  jana  wakati wa  maadhimisho hayo, Amina ,amesema kuwa Manispaa ya Morogoro ni miongoni mwa Manispaa ambazo hazina shida ya vyakula, hivyo  si sahihi Kata ya Kilakala   ikawa  na tatizo la udumavu  wakati  chakula kipo  cha kutosha .

"  Kwanini  Kilakala   tuendelee   kuwa na uduamavu  wakati tunalima matunda ya kutosha  ,tuna wanga wa  kutosha na mboga za majani  za  kutosha  tuna kila aina  ya  virutubisho  vya  mwili  tumekuwa na changamoto  ndogo ndogo  ambazo  zilikiukwa  toka zamani  ila sasa  ni wakati mzuri  wa  kuzifanyia kazi changamoto  hizo " alisema 

Alisema  moja kati ya   changamoto  kubwa  ya baadhi ya  wazazi  kutozingatia  utunzaji mzuri wa  watoto  wakati  wakiwa na ujauzito  na baada ya  ujauzito   kwa kushindwa   kulea watoto  kwa  kipindi cha siku  1000  kama    inavyotakiwa  kwa  mtoto kutunzwa  .
 
Amina,   alisema kuwa suala  lishe  limekuwa na  tatizo mtambuka  katika  Taifa ,  hivyo  ni  wajibu   kwa wadau  wote  ndani ya Kata ya Kilakala   kupambana na suala  la  lishe .

Kuwa  taifa   linapokuwa na  watu  wengi  wenye udumavu ni hatari  sana kwa Taifa  linakosa   watenda kazi  wazuri  hivyo ni lazima   kujipanga  kuona suala la  lishe  linapewa  kipaumbele kama  njia ya  kuondokana kabisa na changamoto ya  lishe  na udumavu  ndani ya  Kilakawilaya .

Alisema  hali ya  lishe  inapaswa   kuongezwa   zaidi ili  kuona jamii  inatumia  vema  vyakula vinavyo zalishwa  katika   wilaya  hiyo  kama  sehemu  ya kuongeza  lishe  bora kwa  jamii .

Akizungumza kwa njia ya simu, Diwani wa Kata ya Kilakala,Mhe. Marco Kanga, alisema  kuwa sababu kubwa inazosababisha hali hiyo ni kutowekeza muda wa kuwa na watoto kuwalisha ipasavyo ikiwepo kuwapa pombe kwa baadhi ya maeneo, lishe duni kutokana na wananchi kutokuwa na elimu ya ulaji wa chakula cha kutosha na chenye mchanganyiko wa viini lishe.

Kanga, alisema  kuwa  kuwa kutokana na changamoto hiyo, Kata ya Kilakala , inatarajia kuweka  mikakati mbalimbali katika kuweza kupambana na hali ya utapiamlo na udumavu kwa watoto wenye chini ya miaka mitano ikiwemo kutoa elimu ya nadharia na vitendo kwa jamii kuhakikisha kwamba ulaji wa kiwango cha juu cha virutubishi unafanyika na kuzingatia unyonyeshaji katika siku 1,000 za mtoto unafuatwa.


No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.