Header Ads

MKURUGENZI MANISPAA YA MOROGORO ATAKA MWALIMU NYERERE AENZIWE KWA VITENDO


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba.


VIONGOZI wa vyama vya Siasa wametakiwa kuiga kwa vitendo uzalendo na moyo wa kujitoa  aliokuwa nao Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere enzi za uhai wake  ili kuliwezesha Taifa kupiga hatua kimaendeleo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, wakati akiendelea kuweka  msisitizo wa nidhamu kazini .

Ameeleza kuwa maisha aliyoishi Baba wa Taifa ni mfano wa kuigwa na viongozi na watanzania wote hasa pale alipojitofautisha na viongozi wengi wa Bara la Afrika alipoepuka tamaa ya madaraka na mali kwa  manufaa ya taifa.

“Serikali yetu ya awamu ya tano chini ya Mhe. Rais Dkt John Magufuli  imekuwa katika mstari wa mbele kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo , hata mimi napenda kusisitiza uwajibika,uzalendo,uandilifu na nidhamu katika kulitumikia taifa la Tanzania kama mnakumbuka  mwalimu alikuwa anapenda kutumia neno (it can be done play your part) kila mtu atimizi majukumu yake” Amesema Sheilla.

Amesema kuwa kumbukumbu za Baba wa Taifa zilizohifadhiwa vizuri katika makumbusho hiyo zina mambo mengi ya kujifunza ambayo wanasiasa wanatakiwa kuyafanya kwa  vitendo hasa  uzalendo kwa nchi, uvumilivu, upendo  na moyo wa kujitoa kwa dhati kuwatumikia wananchi.

“Kupitia kumbukumbu hizi sisi watumishi tumejifunza ukomavu wa demokrasia aliokuwa nao Mwalimu Nyerere akiwa ndani na nje ya Bara la Afrika,  wengi wanadhani Demokrasia ni wakati wa uchaguzi tu, kumbe demokrasia ni pamoja na kuheshimu watu wengine,sote ni mashahidi kupitia kumbukumbu zake tumeona mahali alipokuwa anaishi mwalimu kabla hajajengewa nyumba na Jeshi  kama Rais mstaafu wengi walitegemea asingeishi katika  eneo lile, kumbukumbu hii nzuri aliyoiacha inatufundisha watanzania kuwa mwalimu aliitanguliza Tanzania mbele kuliko maslahi yake binafsi” Amesisitizia  Sheilla.


Sheilla, amebainisha kuwa  serikali itaendelea  kumuemzi Baba wa Taifa kwa yale aliyoyafanya na kuyasimamia kwa manufaa ya taifa huku akitoa wito kwa  viongozi wa vyama vya Siasa wawe na kiasi na waridhike na vile walivyonavyo.

Amempongeza Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kwa kumuenzi vyema Mwalimu Nyerere katika kuimarisha misingi mizuri ya kazi ikiwamo uaminifu, uadilifu na kupinga vitendo vyote vya rushwa pamoja na kuibua miradi mikubwa itakayoiletea Tanzania maendeleo makubwa kuelekea uchumi wa kati na Tanzania ya Viwanda.


Aidha,  amemalizia kwa kuwataka watendaji wote wa serikali ya Halmashuri ya Manispaa ya Morogoro,  kufanya kazi kwa uaminifu,uadilifu,kuwajibika kwenye majukumu yao na kujituma na kamwe hata kuwa tayari kuwavumilia watendaji ambao ni wazembe kazini.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.