Header Ads

MBUNGE ABOOD AKABIDHI VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA MILIONI 10.3 KWA ZAHANATI 5 MANISPAA YA MOROGORO


MBUNGE wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mhe. Abdulaaziz Abood,  amekabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 10.3 kwa Zahanati 5 Manispaa ya Morogoro kupitia fedha za Mfuko wa Jimbo.

Ugawaji wa Vifaa Tiba umefanyika Oktoba 30-31/2023  kwenye Zahanati 4 na Kituo cha Afya 1  ikiwemo Zahanati ya Sultan Area, Zahanati ya Kiwanja cha Ndege, Zahanati ya Mbuyuni, Zahanati ya Kihonda Maghorofani  na Kituo cha Afya Sina Kata ya Mafisa.

Miongoni mwa Vifaa Tiba vilivyotolewa katika Zahanati hizo, ni Darubini 5 (Microscope), Kifaa cha kutenganisha selamu na seli za damu ( Centrifuge Mashine 5), Kifaa cha kupimia sukari ( Glucopus ) 5, Kitanda cha kumuangalia mgonjwa  (Examination  bed 2)  pamoja na Jiko Dogo la Gesi 1.

Mhe. Abood, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wanawake wa Jimbo la Morogoro Mjini,  wanajifungua kwenye mazingira salama.

Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe Manispaa ya Morogoro, Dkt. Maneno Matawa,  amewashukuru Mbunge Abood, kwa Mchango wake hususani kwenye  sekta ya afya huku akieleza kuwa  Vifaa vyote tiba ambavyo wamevipokea vitakwenda kufanya kazi kama ilivyokusudiwa pamoja na kutoa huduma bora kwa wananchi na kuahidi  kuvitunza vifaa hivyo ili viweze kukidhi mahitaji ya wananchi.

Naye Katibu wa Mfuko wa Jimbo la Morogoro Mjini, Elizabeth Badi, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro amesema kuwa Manispaa itaendelea kuunga mkono juhudi za  Serikali pamoja na Ofisi ya Mbunge  katika kuboresha naisha ya wananchi kwa kutoa elimu za kuelimisha jamii kuhusu afya kwa kutumia vikundi mbalimbali vya sauti za umma, kuwapa semina wataam wa afya na kutoa vifaa kwaajili ya Zahanati zote.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.