Header Ads

MBUNGE ABOOD , AWATAKA UWT MOROGORO MJINI KUBUNI NA KUANZISHA MIRADI ENDELEVU YA KUSAIDIA JAMII.

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mhe. Abdulaziz Abood, akipokea Cheti cha Shukrani kutoka kwa Mwenyekiti wa UWT CCM Morogoro Mjini, Victoria Saduka .
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mhe. Abdulaziz Abood,akionyesha cheti cha shukrani alichopewa na UWT Wilaya ya Morogoro Mjini kwa kutambua mchango wake katika chama na kwa jamii.
Mwenyekiti wa UWT CCM Morogoro Mjini, Victoria Saduka akipokea Cheti cha Shukrani kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mhe. Abdulaziz Abood.
Katibu wa UWT CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Rehema Malindi (kulia) akipokea Cheti cha shukrani kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mhe. Abdulaziz Abood.
Katibu wa CCM Jimbo la Morogoro Mjini, Sofia Kibaba, akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi CCM Jimbo la Morogoro Mjini.
             
             

UMOJA wa Wanawake Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM , Manispaa ya Morogoro  wametakiwa kubuni miradi ya kimaendeleo kwa lengo la kupunguza kuomba misaada na kubwa zaidi kujiimarisha kwenye uchumi ili kuunga mkono kauli mbiu ya Uchumi wa viwanda.

Kauli hiyo imetolewa na Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mhe. Abdulaziz Abood, leo Desemba 30/2020 katika Mkutano Mkuu wa Viongozi wa Matawi na Kata wa UWT CCM Wilaya ya  Morogoro Mjini katika Ukumbi wa Mango Garden Manispaa ya Morogoro.

 

Akizungumza na Waandishi wa habari, Mhe. Abood, ameitaka UW T Wilaya ya Morogoro Mjini, kubuni miradi na kuendeleza miradi waliyonayo kama jumuiya nyingine zinavyo fanya na kuwataka kuwa na miradi yao binafsi ili kupunguza tabia ya kutembea na mabakuli kuomba.

 

Mhe. Abood, amesema kuwa ,CCM imekuwa ni taasisi bora ya kisiasa inayotekeleza miradi endelevu inayogusa maisha ya wananchi wa ngazi zote katika jamii.

 “Chama Cha Mapinduzi CCM kitaendelea kuaminiwa na Wananchi wa Morogoro Mjini kama nguzo na kimbilio la kupata Majawabu ya uhakika kwa matatizo yanayowakabili, hivyo niwaombe Viongozi wa Jumuiya hii mshikamane , uchaguzi umekwisha, mimi Mbunge wenu kwa kushirikiana na Chama nitahakikisha Jumuiya hizi zinakuwa na shughuli za kufanya kwa kubuni miradi mbalimbali, jukumu letu sisi  viongozi ni kuhakikisha tunawasaidia kuwawezesha ili kuanzisha vikundi vya ujasiriamali na kuanzisha viwanda ambavyo vitatoa ajira "Amesema Mhe. Abood.

Katika hatua nyengine, Mhe. Abood, ameahdi kutoa fedha katika Jumuiya hiyo ili wabuni mradi mbalimbali  itakayoweza Jumuiya hiyo kusimama yenyewe katika kukabiliana na mfumo tegemezi na kuweza kujikwamua  na umasikini.

Mwisho, Mhe. Abood, amesema uchaguzi umeisha kilichobakia ni Viongozi kuweka nguvu moja katika kuwatumikia Wananchi na kufanya vile walivyoahidi ili kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020-2025.

Katibu wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Sofia Kibaba, amewataka Viongozi walioshinda wtekeleze kikamilifu ahadi zao ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Kibaba, amesema kilichobakia sasa baada ya uchaguzi ni kuhakikisha Jumuiya zinajengwa na kuongezewa nguvu ili zizidi kuimarika.

 

“ Kama alivyosema Mbunge wetu suala la miradi haliepukiki, lengo la miradi kusaidia kazi za Chama zifanyike kwa ufanisi zaidi kuliko kutegemea mifuko ya watu , kama tusipokuwa na miradi hatutokuwa wakali na tutaendelea kubakia dhaifu lakini kama tuna miradi tutakuwa wakali hata katika kusimamia maamuzi yetu na kusongesha chama mbele “ Amesema Kibaba.

Hata hivyo, Kibaba, amesema kutokana na agizo lililotoka ngazi za juu, amewataka Viongozi wote ambao wanavyeo viwili baada ya uchaguzi kwa mujibu wa agizo wanatakiwa kuoandika barua ya kujiuzuru cheo kimoja  ili waachie watu wengine waendelee kushika nyadhifa hizona zoezi la uchaguzi lilatolewa taarifa ili watu waanze kuchukua fomu.

Pia amewataka wale wote waliokosa nafasi katika kinyang’anyiro cha uchaguzi wa ndani ya Chama , wasikate tama kwani chama kina nafasi nyingiza kufanya kazi.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya  Morogoro Mjini,  Bi. Victoria Saduka,  amesema wao wamejipanga kufanya siasa za uchumi na si siasa za maneno .

Saduka, amesema kuwa katika kuona hilo linafanikiwa atahakikisha kupitia Viongozi wa Jumuiya hiyo wataanzisha miradi pamoja na kutoa elimu ya ujasiriamali  kwa Jumuiya hiyo ya UWT ili wajiajiri katika masuala ya ujasiriamali.

Amemuomba Mhe. Abood, kuendelea kuwashika mikono Wakina mama kwani wao walikuwa katika mstari wa mbele  kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi kinaendelea kushika dola hususani katika kuhakikisha Mhe. Abood anarudi madarakani.

“Mhe. Abood, katika watu waliojitoa kuhakikisha unarudi madarakani, UWT hawa wakina mama wamefanya kazi usiku na mchana kuhakikisha unapita kwa kishindo, asilimia kubwa ya kula zimetokana na wakina mama, tunakuomba usituache tushike mkono kwani wakina mama hawa wana imani kubwa sana na wewe hivyo tunaamini uwezo unao utawasaidia ili kufikia malengo” Amesema Mama Saduka.

Naye Katibu wa UWT CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Rehema Malindi, amewataka Wanawake kuwa mfano bora wa kufanya kazi kwa kujiamini ili kujikwamua kiuchumi.

Malindi, amesema kuwa UWT Wilaya ya Morogoro Mjini, wamekuwa katika mstari wa mbele katika  kujitokeza kwa wingi katika masuala mbali mbali ya kuimarisha CCM na Jumuiya zake.

“ Leo tumeitana hapa lakini lengo kubwa ni kumpongeza Mhe. Abood , kwa kupata kura za kishindo na kufanya Jimbo letu kuongoza Kitaifa kwa kura nyingi za Mhe. Rais, hii inatupa faraja kwamba Morogoro tumekuwa kioo kwa Taifa, uchaguzi umekwisha nguvu zetu tuzielekeze katika kujenga Jumuiya zetu, tunaye Mbunge makini tumtumie vizuri ili tujenge fursa mbalimbali katika Jumuiya “ Amesema Malindi.

Shughuli hiyo ilienda sambamaba na Mkutano wa Baraza la UWT Wilaya ya Morogoro Mjini huku ikishuhudiwa tukio la Viongozi kupewa vyeti vya shukrani kutokana na kujitoa kwao katika kazi mbalimbali ndani na nje ya CCM .

 

 

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.