Header Ads

DIWANI KILAKALA AWATAKA VIJANA KUTUMIA MICHEZO KUDUMISHA AMANI NA MSHIKAMANO.

Mhe. Diwani Kata ya Kilakala , Marco Kanga ,akiwa pamoja na Timu na Viongozi wa Kata  katika picha ya pamoja.




DIWANI wa Kata ya Kilakala, Mhe. Marco Kanga, amewahimiza vijana Kata ya Kilakala   kutumia michezo ili kuimarisha amani, upendo na mshikamano.

Kauli hiyo ameitoa leo Desemba 04/2020 kwenye Uwanja wa  kwa Winga Kilakala , wakati wa hafla fupi ya pongezi ya timu ya Mpira wa Miguu ,Nughutu FC , baada ya kuibuka kidedea katika fainali ya mashindano ya Jezi  yaliyofanyika Novemba 29/2020 katika Viwanja vya Sabasaba.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, ambapo Vijana walikusanyika kwa lengo la kushiriki katika hafla hiyo ,Kanga , ameeleza kuwa michezo imekuwa ikitumika kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha ushirikiano na kuwajengea vijana uzalendo.

“Kupitia michezo mnayofursa kama vijana kuendelea kuenzi falsafa za waasisi wa taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Hayati Mzee Abeid Amani Karume ambao walikuwa wazalendo kwa taifa lao na waliimarisha muungano kwa maslahi ya watanzania wote, niwatoe hofu nitasimama bega kwa bega na  nyinyi katika kuhakikisha michezo katika Kata yetu inakuwa namba moja, mlionenyesha imani na mimi mkanipatia ridhaa ya kuwa Diwani wenu, basi mimi nitatekeleza kwa vitendo ,” Amesema Kanga.

Kanga, amesema  kuwa michezo hiyo iliyowakutaisha vijana ikatumike kama sehemu ya kuwa na amani, uvumilivu na mshikamano.

 

“Hiki mlichokifanya kimeleta fahari sana katika Kata yetu, nimpongeze sana Mwenyekiti wa Mtaa wa Nughutu ,amefanya kazi kubwa sana ya kujitoa na kupata ushindi, lakini sitowasahau wadau mbalimbali ambao walikuwa pamoja nasi katika kufanikisha timu yetu inafanikiwa kuchukua ubingwa, kikubwa mtambue kwamba Vijana mnatakiwa kujenga taifa kwa vitendo vinavyodumisha amani, upendo na mshikamano kama ambavyo Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere alivyotujengea taifa lenye umoja,” Ameongeza Kanga

 

Aidha ,  amewasihi vijana kutambua wajibu wao katika jamii na kuifanya michezo kuwa ni miongoni mwa mambo muhimu wanayopaswa kuyaendeleza katika kutekeleza mipango waliyonayo.

 

Katika hatua nyengine, Kanga, ametoa kiasi cha Shilingi 200,000/= kwa ajili ya kuwapa motisha Vijana kuendelea kujituma zaidi  na kuiletea heshima Kata ya Kilakala katika Nyanja za michezo.

 

Mbali na fedha, pia ameahidi kuikabidhi timu hiyo mbuzi 2 katika kikao cha wadau kitakachofanyika siku za usoni ikiwa ni zawadi kwa niaba ya Ofisi ya Kata, Ofisi ya Chama pamoja na Wananchi wa Kilakala.


Hata hivyo, amewataka na kuhimiza Vijana kuunda  vikundi kwa ajili ya kupatiwa mikopo ya Halmashauri inayotolewa ya asilimia 10 huku gharama za usajili akiahidi kuzibeba yeye.

 

Mwisho, amesema kabla ya kumalizika kwa mwaka huu, yupo mbioni kuanzisha Kombe la Kanga CUP, litakaloshirikisha timu za mitaa yote ndani ya Kata ya Kilakala ambapo washidni watapewa zawaidi kubwa kabambe ambayo bado imekuwa ni siri mpaka pale mashindano yatakapo tarajia kuanza.

 

Kwa upande wake, Katibu wa CCM Kata ya Kilakala, Scolastica Mwanyika,  amesema kuwa michezo imekuwa na umuhimu wake  ikiwa ni njia moja wapo ya kuwaendeleza vijana ili waweze kuimarika kiafya na kiakili.

“Michezo ni moja ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) , hivyo kwa kutambua hilo sisi Viongozi wa Chama kwa kushirikiana na Viongozi wa Serikali , tutakuwa bega kwa bega  katika kuinua viwango vya michezo, lakini niwaombe tuzitumie hizi nafasi kwani michezo kwa sasa ni ajira kama zilivyo ajira nyengine, lakini kikubwa zaidi tusijihusishe na vitendo vya uharaifu kwani vitatusababishia kuharibu mfumo wa maisha yetu kwa kupoteza maisha au kuishia jela””Amesema Scolastica.

Mwisho , amesema yupo tayari kuchangia kuhakikihsa kwamba Kata ya Kilakala inakuwa vinara katika michezo mbalimbali Manispaa ya Morogoro.

Naye Mtendaji wa Kata ya Kilakala, Amina Said, ameahidi kuwapatia Vijana hao mipira katika kukabiliana na changamoto ya mipira wanayokumbana nayo hivi sasa.


 

 

 

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.