Header Ads

DIWANI KILAKALA AKABIDHI MIFUKO 10 YA SARUJI NA KUWATAKA WANANCHI KUCHANGIA SHUGHULI ZA MAENDELEO.

                     

Diwani wa Kata ya Kilakala Mhe. Marco Kanga (wapili kutoka kulia) akikabidhi mifuko ya Saruji 10 kwa ajili ya ujenzi wa Kivuko kinachounganisha Mtaa wa Bong'ora na Mbogo .

                   

                   

Diwani wa Kilakala, akiwa na timu ya Viongozi wa Ngazi ya Mtaa wa Bong'ora mara baada ya makabidhianao ya Saruji.

                 

Kivuko kinachoendelea na ujenzi kinachounganisha Mtaa wa Bong'ora na Mtaa wa Mbogo.

                           
  
Diwani wa Kilakala, Mhe. Marco Kanga, akishiriki kuchimba msingi wa ngazi katika ujenzi wa madarasa mapya 4 ya Shule ya Sekondari Mazoezi- Lupanga .
Diwani wa Kata ya Kilakala Mhe. Marco Kanga, akikagua ujenzi wa madarasa.
                

DIWANI wa Kata ya Kilakala, Marco Kanga, amewataka wananchi wa Kata ya Kilakala kuwa na desturi ya  kuchangia na kujitolea nguvu kazi kwenye ujenzi wa miradi ya kijamii hali itakayowafanya kupiga hatua kimaendeleo katika maeneo yao.

Kauli hiyo ameitoa leo Desemba 31/2020 wakati wa Ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo ikiwamo Ujenzi wa Kivuko kinachounganisha Mtaa wa Bong’ora na Mtaa wa Mbogo Kata ya Kilakala pamoja na Ujenzi wa Vyumba 4 vya madarasa Shule ya Sekondari Mazoezi -Lupanga.

Kanga, amesema kuwa viongozi wa ngazi zote kwa kushirikiana na wananchi wanapaswa kushiriki katika kuchangia na kuhamasishana kuchangia maendeleo kwani Diwani  peke yake awezi kufanikisha mambo yote katika Kata.

Aidha, amesema kuwa maendeleo hayana chama, hivyo wananchi na viongozi wanapaswa kuwa wamoja kwa sababu watakao tumia miradi hiyo ni watu wote bila kujali itikadi za kisiasa .

‘’katika maendeleo hatuangalii vyama, kwa kuwa wanufaika wa miradi hii ni wananchi wa Kata yote ya Kilakala, Nampongeza sana dada yangu Afisa Mtendaji wa Kata ya Kilakala, Watendaji wa Mitaa pamoja na Viongozi wa Serikali za Mitaa  kwa namna mlivyohamasisha wananchi kushiriki kuchangia ujenzi wa miradi mbali mbali katika Kata yetu ikiwamo huu wa Kivuko ambapo zaidi ya Milioni moja  1,000,000/= wananchi wamechangia kufanikisha hatua hii ya ujenzi iliyofikiwa” Amesema Kanga.

Katika ziara hiyo, Mhe. Kanga, amekabidhi jumla ya Mifuko 10 ya Saruji yenye thamani ya Shilingi 160,000/= kwa ajili ya ujenzi  wa Kivuko hicho kinachojengwa  kwa nguvu za wananchi ili kuweza kuwapatia hamasa wananchi wake katika suala la uchangiaji wa maendeleo.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Bong’ora ,Yusta Medadi, amewataka Viongozi wa Mtaa wa Bong’ora kusimamia ipasavyo ujenzi waKivuko hicho ili kutowavunja moyo wananchi walioshiriki katika ujenzi huo.

“Tunamshukuru sana Diwani wetu kwa kutupatia mifuko hii 10 ya Saruji kwa ajili ya kivuko kinachounganisha Mtaa wa Bong’ora na Mbogo, kwakweli barabara ni changamoto , wananchi wamejitolea lakini tunamshukuru sana Mhe. Diwani kwani sio mchango wake wa kwanza ameshachangia kiasi cha fedha hadi hatua hii tuliyofikia, kikubwa  amewaomba Viongozi wa Serikali ya Mtaa wa Bong’ora kusimamia ipasavyo ujenzi wa Kivuko hicho ili kutowavunja moyo wananchi walioshiriki katika ujenzi huo” Amesema Medadi.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Bong’ora , Bi Pokea Mrisho, ameshukuru kupata msaada wa Saruji huku akimtaka Diwani huyo kuendelea na moyo wa kujitolea kwa ajii ya maendeleo ya Wana Kilakala pamoja na wananchi wa Mtaa wa Bong’ora.

Kwa upande wa Mwananchi wa Mtaa wa Bong’ora, Steven Konea, amewaomba  Wadau na Viongozi kuongeza nguvu ya kuwasaidia kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Kivuko hicho na kivuko chengine  pamoja na kuimarisha barabara hiyo kwani hata udongo uliopo barabara hiyo unahitaji vifusi ili magari na malori yaweze kupita vizuri.


 

 

 

 

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.