Isco mikononi mwa Mourinho
Manchester City wanaamini wanaweza kusaini makataba na mchezaji wa kiungo cha kati wa Real Madrid Mhispania Isco msimu huu wa majira ya joto. Mkataba kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 unaweza kuwa wa thamani ya Euro milioni 75. (Mirror)
Mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski, mwenye umri wa miaka 29, atawasilisha maombi yake ya kutaka kuhamia Real Madrid msimu huu wa majira ya joto. Mchezaji wa Chelsea mwenye umri wa miaka 25 na mchezaji wa kimataifa wa Uhispania Alvaro Morata ni mmoja wa washambuliaji ambao Bayern Munich inamtaka kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Pole iwapo watampoteza. (AS - in Spanish)
Meneja wa Watford Javi Gracia amemkosoa Abdoulaye Doucoure, mwenye umri wa miaka 25, kwa kukataa kuhama katika msimu huu wa majira ya joto, huku Manchester United Tottenham, Liverpool na Arsenal kwa pamoja wakimthamanisha mchezaji huyo wa kiungo cha kati kwa kiwango cha Euro milioni 40. (Mail)
Post a Comment