Header Ads

MANISPAA YA MOROGORO YAMKABIDHI SHILINGI 300,000/= MKAZI WA KATA YA CHAMWINO ALIYEUNGULIWA NA NYUMBA.



Said Mwele (kulia) akikabidhiwa kiasi cha Shilingi 300,000/=


MANISPAA ya Morogoro, imemkabidhi Mkazi wa Kata ya Chamwino Mtaa wa Chamwino, Said Seif Mwele, kiasi cha Shilingi 300,000/= kufuatia kuunguliwa na nyumba yake.

Akikabidhi fedha hizo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Mchumi Manispaa ya Morogoro, Happines  Masatu, amesema fedha hizo zimetolewa kufuatia mkazi huyo kuunguliwa na nyumba na kupoteza mali zote.

Masatu , amesema baada ya kupewa taarifa kupitia Mtendaji wa Kata ya Chamwino, Ofisi ya Mkurugenzi ilifika katika eneo hilo na kumuahidi mkazi huyo kumsaidia ili aendelee kujikimu na maisha.

“Tulipokea taarifa kutoka kwa Mtendaji wa Kata, ambapo mkazi huyo aliunguliwa na Nyumba tarehe 25 /09/2020 , baada ya taarifa hiyo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro aliagiza kijana huyo kupatiwa fedha ili aweze kujikimu kwani amepoteza kila kitu , kwahiyo leo tumemkabidhi fedha aliyoahidiwa “ Amesema Masatu .

Kwa upande wa,  Said Mwele,  amemshukuru Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kwa kuonyesha moyo wa kujali.

“Kweli nimepatwa na majanga makubwa sana, lakini namshukuru sana Mkurugenzi wetu kwa kuonyesha kuguswa na matatizo ya wananchi wake, hiki alichonipatia ni kikubwa kwangu kwani huu ni msaada , naimani sasa nitavaa angalau nguo maana tangia tukio litokee sina nguo za kubadili wala mahala  kwa kulala , nina watoto 3 na mke wangu, kikubwa ni shukrani ni viongozi wachache wenye moyo kama huu” Amesema Mwele.


 

 

 

 

 

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.