Header Ads

Waliopata mafunzo ya jeshi la Akiba (Mgambo) Wilaya ya Morogoro watakiwa kuwa wazalendo.








MKUU  wa Wilaya ya Morogoro, Bakari Msulwa, amewaasa  Vijana kuwa wazalendo wa nchi yao kwa kuacha kujiingiza katika viashiria vya uvunjifu wa amani ili kusaidia kuepukana na migogoro itakayopelekea uvunjifu wa Amani.

Hayo ameyasema leo Novemba 25/2020 wakati kufunga  rasmi mafunzo hayo yaliyofanyika katika  Uwanja wa mpira wa miguu wa Jamhuri.

Msulwa, amesema kuwa itakuwa ni fedheha kwa taifa ikibainika kuwa vijana hao waliopikwa kwa misingi ya uzalendo wameshiriki katika matukio ya ujangili na migomo  isiyo na tija au kutumika kisiasa.

Katika hatua nyengine, amewapongeza wahitimu wote na kuwasihi kuyatumia mafunzo hayo kama chachu ya kujiletea maendeleo na kuhakikisha kuwa wanailinda jamii inayowazunguka.

 Aidha, amewaahidi kuwa Serikali ipo nao bega kwa bega na ndiyo maana imetumia gharama kubwa kuwapatia mafunzo hayo.

Hata hivyo, ametumia fursa hiyo kuyaomba makampuni binafsi ya ulinzi kuwatumia vijana hao wenye mafunzo ya kijeshi kwa shughuli zao za ulinzi. 


Pia, ametumia fursa hiyo kuwaasa vijana wilayani humo kuwa inapotokea fursa kama hiyo wajitokeze kwa wingi na wasikatishwe tamaa kwani Serikali inatumia gharama kubwa kufanikisha mafunzo hayo.


"Vijana wangu najua mmepitia vikwazo vingi na ninajua mlikatishwa tamaa maana wapo mabingwa wa kukatisha watu tamaa lakini mmevuka salama na leo mnahitimu, basi mafunzo haya yawe na tija katika maisha yenu binafsi na jamii inayowazunguka". Amesema DC Msulwa.

 
Mafunzo hayo ya miezi 4  yamejumuisha jumla ya Vijana 200  chini ya usimamizi wa Mshauri wa Jeshi la Akiba Wilaya ya Morogoro.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.