Header Ads

AJIRA JUMUISHI- WALEMAVU WASIWE WA ZIADA.

 


WATU  wenye ulemavu Tanzania ni kundi dogo la watu wasiozidi hata 2,000,000 kwa bara na visiwani ila ni kundi linaloongoza kutaabika mitaani ukiachana na Makundi ya Wagonjwa,Wafungwa na Wakimbizi hapa Tanzania.

Kumekuwa  na changamoto kubwa sana katika jamii na taasisi zetu juu ya watu wenye ulemavu kutoweza kushiriki kwa pamoja katika ajira  jumuishi hii imetokana na mitazo tofauti toafauti juu yao.

Lakini, suala la walemavu kutokuingia katika ajira jumuishi limekuwa kikwazo kwao kwani wengi wao wamekuwa wakiishi katika maisha tegemezi jambo ambalo limekuwa likiwaathiri kisaikolojia na kuathiri mazingira yao na hata kufikia wakati kutojiona kwamba wao sio sehemu ya jamii kutokana na kutengwa kwao.

Hali ya wanawake na wanaume walemavu kwenye soko la ajira linatia hofu na mashaka makubwa kwani wana fursa ndogo zaidi ya kuajiriwa kuliko wasio walemavu na hata wakiajiriwa wengi wao huwekwa katika sekta ambazo malipo yake ni haba.

Sekta ya Ajira.

Tanzania kupitia jitihada za Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Awamu ya Nne, iliweka sheria maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu ijulikanayo kama "Sheria ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2010".

Katika sheria hiyo baadhi ya mambo mazuri yaliainishwa yahusianayo na masuala ya Ajira kwa Watu wenye ulemavu hususani kwenye Ibara ya 31 na 32.

Ikumbukwe kwamba, katika Sheria namba 9 ya Ajira ya mwaka 2010 inasema,“Mwajiri yoyote awe wa Umma au Binafsi mwenye waajiriwa kuanzia 20 na kuendelea lazima asilimia 3 ya waajiriwa hao iwe kwa ajili ya watu wenye ulemavu” hii inaonyesha kuwa walemavu wana haki ya kuajiriwa mahali popote.

Tujiulize mambo yafuatayo? 

1.Kila Mwajiri mwenye wafanyakazi ama Waajiriwa kuanzia 20 na kuendelea ahakikishe 3% kati ya hao wawe ni watu wenye ulemavu(kwa taasisi Binafsi na za umma)
Swali :
-Ni Taasisi ngapi za Serikali zenye jumla ya wafanyakazi 300ambao kati ya hao 9 ni watu wenye ulemavu???

-Ni taasisi ngapi za binafsi zinafanya hivo??

-Je Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma kama chombo pekee kinachoratibu michakato ya Ajira serikalini kinawajibikaje kwa Waajiri wa taasisi za Umma ili kuhakikisha sheria hii inatekelezwa kikamilifu??

-Je ni kweli kwamba Sekretarieti ya Ajira katika utumishi wa umma hausiki kwa namna yoyote ile na utekelezaji wa sheria hii kama anavodai Naibu Katibu wake???
2.Kila mwajiri ahakikishe anapeleka ripoti ya utekelezaji wa sheria ya watu wenye ulemavu kuhusu waajiriwa wake ambao ni watu wenye ulemavu kwa Kamishna wa Kazi kila mwaka.

Swali :
-Ni waajiri wangapi wa taasisi Binafsi na Umma wanawasilisha ripoti hizo kwa Kamishna kila mwaka??

-Kama jibu ni ndiyo je huwa wanawasilisha ripoti sahihi kwa kkiasi gani??
-Je ripoti hizo huwa zinafanyiwa kkazi ??

-Kama jibu ni ndiyo kwann idadi kubwa ya watu wenye ulemavu wasio na Ajira inazidi kuongezeka kila kukicha??

-Je waajiri huwa huwa wanakaguliwa kuhusiana na utekelezaji wa sheria hii ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2010,Sheria ya kazi ya mwaka 2004 na Mkataba wa kimataifa wa Watu wenye ulemavu wa mwaka 2010??

Bado naendelea kutoa na kuwahamasisha  walemavu kuchangamkia fursa za ajira zinazotangazwa na Ofisi ili waweze kupata fursa .

Katika kuona Soko la ajira linakuwa Jumuishi kwa watu wenye ulemavu ni shauri kuwa ni vyema walemavu kuzitaja changamoto zao kweye fomu za maombi ili Ofisi husika  iweze kuwaandalia mazingira rafiki kwa ajili ya mchakato mzima wa upatikanaji wa ajira na baada ya kupata ajira waweze kupangiwa sehemu ambazo hazitakua changamoto kwao.

Katika kuona suala la ajira Jumuishi linakuwa ajenda ya watu wenye ulemavu, lazima sasa Walemavu pia wajione nao ni sehemu ya  kuchangia maendeleo ya Nchi na kutumia fursa mbalimbali zinazojitokeza ili kujikwamua kiuchumi.

Sekta ya Maendeleo ya Jamii.
Bado kuna changamoto za kisera hapa, ukiangalia katika mfuko wa uwezeshaji kiuchumi, asilimi 10 ya mapato ya ndani ambayo inatumika asilimia 2 % ya watu wenye ulemavu licha ya Serikali kusikia kilio cha wanaharakati na kuanza  kubadili sheria ambayo kwa sasa mlemavu 1 anakopesheka peke yake tofauti  na awali hadi wawe katika kikundi jambo ambalo lilikuwa likiwanyima fursa walemavu kutokana na masharti ya walemavu kwanza kuishi mtaa mmoja na Kata moja hali iliyowapelekea walemavu wengi kushindwa kukidhi vigezo hiyo.

Baada ya mabadiliko hayo, Serikali ilifanya maboresho ya sheria na sasa walemavu wanakopa kuanzia mtu 1 na kuendelea bila kuangalia Mtaa wala Kata kwa makundi kama ilivyokuwa awali.

Lakini licha ya maboresho hayo, bado kuna genge la watu wenye ulemavu wa utindio wa ubongo, hili kundi limetengwa sana, hoja yangu ni kwamba Serikali ifikirie upya kundi hili kwa kuweka wawakilishi katika kutumia mkopo wa asilimia 2 ya walemavu ili walemavu wote wawe sawa na kunufaika na mkopo huo na kupunguza wimbi la walemavu wanaongezeka barabarani wanao ombaomba.

Sekta ya elimu.

Mfumo wa elimu maalumu unaweza kuchangia baadhi ya watoto kukosa haki za msingi kutokana na umri lakini pia kupoteza asili na tamaduni zao kwa kusoma mbali na nyumbani kutokana na wazazi wengi kuwapeleka watoto shule maalumu na kuwatelekeza watoto huko.

Hivyo ushauri wangu ni kwamba tuendelee kutoa elimu juu ya kuwepo kwa mfumo wa elimu jumuishi kwa  watoto wenye mahitaji maalumu kuchanganyikana na wengine ujambo ambalo litasaidia sana kutengeneza  umoja na kuondoa unyanyapaa kwa kuwa tayari wamezoeana na kupendana pamoja na kupewa ushirikiano kutoka kwa wenzao.

Mwisho nipende kusema kuwa , ili Walemavu waweze kupewa kipaumbele katika ajira Jumuishi ni lazima pande zote tusimame kama wanaharakati wa kuwatetea kwa hoja zenye nguvu katika kuona ajira Jumuishi inatimia.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.