Header Ads

MAHAFALI YA SABA YA SHULE YA SEKONDARI YA WAVULANA YA SULLIVAN PROVOST YA KIBAHA YAFANA


 Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya Wavulana ya Sullivan Provost,  Rachel Mwalukasa akikabidhi zawadi ya kitabu kwa mmoja ya wahitimu wa kidato cha nne wakati wa hafla ya mahafali ya saba ya shule hiyo iliyopo kibaha kwa mathias mkoni pwani.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya Wavulana ya Sullivan Provost,  Rachel Mwalukasa (katikati), akizungumza wakati wa sherehe za mahafali ya saba ya kidato cha nne ya shule hiyo iliyopo  Kibaha kwa Mathias Pwani, hivi karibuni kushoto ni  Afisa Mradi wa Teachers Juction, Njama Salim, pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Prof. Elifas Tozo Bisanda   ambae ndio alikuwa Mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Prof. Elifas Tozo Bisanda  (wapilikushoto), akimkabidhi mwanafunzi wa Kidato cha kwanza wa Shule ya sekondari ya wavulana  Sullivan Provost  Francis Kiango, cheti cha pongezi kwa kuongoza katika masomo yote wakati wa hafla ya mahafali ya  saba ya shule hiyo, hafla ya mahafali hayo yamefanyika shuleni hapo  Kibaha kwa Mathias, mkoani Pwani hivi karibuni. Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shule hiyo, Rachel Mwalukasa, wengine ni wageni waalikwa pamoja na Baba Mlezi wa kiroho wa shule hiyo  Mshungaji Tusimsahau Manoza pamoja na Mama Manoza.

:Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Prof. Elifas Tozo Bisanda  (wa tatu kushoto) aliyekuwa mgeni rasmi akikabidhi cheti kwa mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne wa Shule ya Sondari ya wavulana ya Sullivan Provost, Rahim Ally (kulia), wakati wa mahafali ya saba ya shule hiyo, hafla ya mahafali hayo yamefanyika shuleni hapo  Kibaha kwa Mathias, mkoani Pwani hivi karibuni. Wengine (wapili kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shule hiyo, Rachel Mwalukasa na  Afisa Mradi wa Teachers Juction, Njama Salim.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.