Header Ads

WADAU WA AFYA WATAKIWA KUENDELEZA MAPAMBANO DHIDI YA USUGU WA VIMELEA VYA DAWA.













WADAU  wa afya wametakiwa kuendeleza mapambano dhidi ya tatizo la usugu wa vimelea vya dawa kwa kuongeza uelewa kwenye jamii na kutia hamasa kuhusu usugu wa dawa za binadamu ambao  unatishia afya za binadamu  duniani kote.

Hayo yamelezwa leo Machi 29/2022 na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dr.Kusirye Ukio, akimwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro katika Semina ya mafunzo ya matumizi sahihi ya dawa zenye asili ya kulevya (Controled drugs) yaliyofanyika katika  Ukumbi mdogo wa Makataba ya Mkoa wa Morogoro iliyopo Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza na Wafamasia walioshiriki katika Halamashauri zote Mkoa wa Morogoro , Dr Ukio, amesema licha ya juhudi za serikali katika kuhakikisha wananchi wake wanakuwa na afya njema bado kuna jitihada binafsi ambazo zinatakiwa kufuatwa zinazozingatia i taratibu za kitabibu katika kutibu wagonjwa kwa kuwapatia dawa kwa  utaratibu maalumu.

" Kuna umuhimu wa elimu zaidi kutolewa kwa jamii ili kuongeza uelewa kuhusu usugu wa dawa za binadamu unaotokana na utolewaji wa dawa kiholela bila cheti cha daktari na kusababisha madhara kwa afya ya binadamu, hivyo nitoe ushauri kwa wadau wa afya hususani wafamasia kuwa na utaratibu wa kutoa huduma baada ya kupokea cheti kutoka kwa Daktari ili kunusuru afya za wateja wetu" Amesema Dr. Ukio.

Dr. Ukio, amesema zipo sababu zinazochangia usugu wa dawa kwa binadamu kuwa ni pamoja na kutumia dawa bila kupima na kupata ushauri  wa kitabibu,kutokukamilisha dozi pamoja na matumizi ya dawa za binadamu kwa mifugo .


Naye Meneja wa TMDA Kanda ya kati zikijumuisha mikoa ya Morogoro, Singida, Dodoma  na Iringa, Bi. Sonia Mkumbwa, amewataka Wafamasia kujenga utaratibu wa kupitia mara kwa mara katika maduka na vituo vyao vya afya kupitia na kuona matumizi ya dawa hizo yanavyotumika kama yanazingatia taratibu au la.

Bi. Mkumbwa, amesema  kuwa  Usugu wa dawa ni hali ya dawa kushindwa kuua vimelea vya magonjwa  au kuzuia ukuaji wake na hivyo dawa kushindwa kudhibiti vimelea hivyo.

" Mafunzo haya muhimu sana kwenu, tunaendelea kukumbushana  ili tuzingatie sheria na miongozi ya matumizi ya dawa hizi kwa wafamasia wetu, lakini nipende kuiambia jamii kuwa vimelea vya magonjwa ndio hujenga usugu wa dawa , jamii inapaswa kupiga vita matumizi mabaya ya dawa, lazima tuwe na  huruma kwa binadamu wenzetu,ikiwa sheria na miongozo ya kiafya itafuatwa itasaidia wafamasia  kufanya kazi kwa weledi ikiwa ni pamoja na utekelezaji  wa sheria za afya”Amesema Bi. Mkumbwa.

Kwa upande wa Mfamasia wa Mkoa wa Morogoro, Bi. Neema Shanalingigwa, amefurahishwa na mafunzo hayo ya matumizi sahihi ya dawa zenye asili ya kulevya, huku akiwataka Wafamasia wote Mkoa wa Morogoro kuhakikisha wanasiamamia vyema  suala la utoaji wa dawa hizo  na kupitia mara kwa mara katika  maduka yote ya dawa ambayo yanatoa huduma za dawa.

Katika hatua nyengine, miongoni mwa Wafamasia akiwemo Mfamasia wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, Joyceline Boniphace, ameseam atahakikisha kwamba mafunzo hayo yanazaa matunda kwani watajipanga kikamilifu kuona dawa zote zikiwemo dawa zenye asili ya kulevya (Controled drugs) ikiwamo Narcotics na Psychotropics  zinafuata utartibu katika matumizi yake.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.