Header Ads

MANISPAA YA MOROGORO YAANZA ZOEZI LA UUZAJI VIWANJA , RC MWASA ATOA KAULI NZITO KWA VISHOKA.







WAKATI Manispaa ya Morogoro ikianza rasmi zoezi la uuzwaji wa Viwanja eneo la Kiegea A na B Star City mara baada ya kumalizika kwa mgogoro uliodumu kwa muda mrefu, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa, amepiga marufuku madalali wa uuzwaji wa Viwanja (Vishoka) ambao wamekuwa vyanzo vya migogoro ya ardhi.

Kauli hiyo ya Mkuu wa Mkoa, ameitoa Novemba 30/2022 wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa mpango wa  kutangaza na kukabidhi Viwanja vilivyopimwa na Manispaa ya Morogoro eneo la Star City Kiegea.

Akizungumza katika uzinduzi huo, RC Mwassa, amewataka wananchi watakaopewa fidia na wale watakaonunua Viwanja marufuku kuuza kiholela Viwanja hivyo kwani kufanya hivyo kunasababisha migogoro ya ardhi.

Aidha, RC Mwassa, amesema mwananchi yeyote atakayetaka kuuza Viwanja vyake lazima awasilishe maombi kwa Mkurugenzi wa Manispaa ikiwa imeonyesha orodha ya Viwanja anavyokusudia kuviuza.

“Migogoro imeisha, wale mabingwa wa kuuza viwanja bila kufuata utarartibu iwe mwanzo na mwisho, vishoka nitakula naoa sahani moja,lazima madalali wa viwanja tuwaondoe, haiwezekani tumetumia nguvu kubwa ya kutatua mgogoro wao waanziishe upya hili sitalivumilia, niombe Manispaa hiki  ni chanzo kipya cha mapato, hakikisheni fedha za wananchi ziingizwe moja kwa moja kwenye akaunti yake wakati wa mauzo ambayo ataiwasilisha Manispaa wakati wa uundaji mkataba” Amesema RC Mwassa.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Albert Masando,amesema kwa sasa Mji unahitaji kupangwa hivyo wananchi lazima wasikilize maelekezo na maagizo ya Viongozi badala ya kukiuka maagizo hayo.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Ally Machela,amesema katika mchanganuo wa matumizi ya viwanja , eneo la makazi Viwanja 2,740, Makazi na Biashara 915, Huduma (Shule, Zahanati, Vituo vya afya n.k) 147,  Biashara 36, Viwanda Vidogo 68 na Maeneo ya wazi (POS) na Viwanja vya Michezo 59. 

Zoezi la Ugawaji wa Fomu za mauzo ya Viwanja litaanza kufanyika Tarehe 5/12/2022 katika Ofisi za Ardhi zilizopo Stendi Mpya ya Daladala Mafiga ambapo kwa malipo ya ununuzi ya Viwanja yatafanyika kwa awamu moja ndani ya miezi 3 na bei ya fomu ni shilingi elfu 20.

                                                                                            

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.