Header Ads

MANISPAA YA MOROGORO YAPONGEZWA UTEKELEZAJI UGAWAJI DAWA ZA KICHOCHO NA MINYOO YA TUMBO.




AFISA  Mpango kitengo cha kichocho na Minyoo ya tumbo Wizara ya afya Mpango wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele,Mohamed Nyati, amesema kuwa   ameridhika na maandalizi ya watoto shuleni   kwani kila shule imewandaa  watoto vizuri kwa kuwa elimisha umuhimu wa kumeza dawa za minyoo ya tumbo na kichocho.

Kauli hiyo ameitoa leo Novemba 15/2022  akiwa katika ziara ya kuzitembelea   shule zilizopo Manispaa ya Morogoro  kwa ajili ya kuangalia mwenendo mzima wa zoezi la ugawaji dawa za minyoo ya kichocho na minyoo ya tumbo kwa wanafunzi wa Shule za Msingi  za Serikali na binafsi.

Nyati,amesema  kuwa utekelezaji wa zoezi hilo unaendelea  vizuri kwani kila shule imeandaa mazingira safi ya kugawia dawa na  pia walimu wamehakikisha  kila mtoto ana pata chakula cha kutosha kabla ya kunywa dawa hizo.

Naye Mratibu wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Manispaa ya Morogoro, Dr.Warialanga Nnko,amewashukuru Waalimu na Wazazi kwa ushirikiano wao katika kufanikisha zoezi hilo.

"Nimeridhishwa na zoezi la ugawaji wa dawa, mpaka sasa hakuna madhara yoyote na changamoto yoyote ambayo imejitokeza, kikubwa niwaombe waalimu wazidi kutoa elimu kwa wazazi ili kufanikisha zoezi hilo" Amesema Nnko.

Mwisho, Nnko, amewasisitiza Walimu hao kuendelea kuwa karibu na  wanafunzi hao  pamoja na kuwapatia elimu  ya kuwaondoa hofu baada ya kunywa dawa  hizo.

Utekelezaji wa  zoezi la ugawaji wa dawa za minyoo ya tumbo na minyoo ya kichocho kwa wanafunzi wenye umri wa miaka  5-14 kwa Shule za Msingi  Manispaa ya Morogoro umeanza  leo Novemba 15/2022 na linatarajia kukamilika Novemba 16/2022  ambapo zoezi hilo linatekelezwa chini ya usimamizi wa walimu wakuu na walimu wa afya kwa kila shule husika.

Miongoni mwa baadhi ya shule zilizotembelewa ni Shule ya Msingi Mkundi, Mgulu wa ndege, Ahmadya, Carmel, Mwenge pamoja na Bensal.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.