Header Ads

WEZESHA MABADILIKO WAIKABIDHI MANISPAA YA MOROGORO CHOO CHA MTOTO WA KIKE.

 

Choo cha Mtoto wa Kike Shule ya Sekondari Uluguru ,kilichofadhiliwa na Taasisi ya WEZESHA MABADILIKO.

Mkurugenzi wa WEZESHA MABADILIKO, Dr. Lusako Mwakiluma (kushoto), akisalimia na Afisa Elimu Taaluma Msingi Manispaa ya Morogoro, Leah Selemani (kulia) mara baada ya uzinduiz wa Choo cha Mtoto wa Kike.

Mkurugenzi wa WEZESHA MABADILIKO, Dr. Lusako Mwakiluma (watatu kutoka kushoto) , Mtendaji wa Kata ya Kihonda Tatu Ally (kushoto) wakiwa na Wanafunzi mara baada ya uzinduzi wa Choo cha Mtoto wa Kike.

Mkurugenzi wa WEZESHA MABADILIKO, Dr. Lusako Mwakiluma (watatu kutoka kushoto),akimkabidhi ndoo ya kunawia maji Afisa Elimu Taaluma Msingi Manispaa ya Morogoro, Leah Selemani (kulia).

TAASISI isiyo ya Kiserikali ya WEZEESHA MABADILIKO chini ya Mkurugenzi wake. Dr. Lusako Mwakiluma,imeikabidhi Manispaa ya Morogoro Choo cha Mtoto wa Kike katika Shule ya Sekondari Uluguru.

Tukio hilo la makabidhiano ya Choo limefanyika hivi karibuni ambapo Choo hicho katika makabidhiano kilipokelewa na Mwakailishi wa Mkurugenzi kutoka idara ya elimu Msingi, Leah Selemani.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi choo hicho, Mkurugenzi wa WEZESHA MABADILIKO, Dr. Lusako, amesema kwa kuwa wanawake wengi wamekuwa na changamoto nyingi katika mabadiliko ya kimwili hivyo wameona kujenga Choo cha Mtoto itakuwa ni suluhisho la kuwaondolea adha wanafunzi wakike wanapoingia katika hedhi.

Dr. Lusako,amesema kuwa tafiti  zinaonesha kuwa mtoto wa kike anakosa masomo siku 4 hadi 5 kila mwezi kutokana na ukosefu wa huduma ya vyoo bora na maji salama na safi shuleni ambapo Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizosaini mkataba wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ifikapo mwaka 2030. Miongoni mwa malengo hayo ni lile lengo namba 4: linalohamasisha kuhusu Elimu Bora, Lengo la 5: linalo hamasisha juu ya Usawa wa Kijinsi na lengo namba 6: kuhusu Maji Safi na Salama.

“Huu ni mwanzo tu bado tuna malengo ya kusaidia na shule nyengine ,  tunataka choo hiki kiwe cha mfano katika Manispaa yetu ya Morogoro , tuliona kuna Choo Tubuyu Sekondari lakini kuna chengine hakijaisha pale Kihonda Sekondari, sisi baada ya kuguswa na jitihada hizi, tumeona nasisi  tuunge mkono jitihada za  Manispaa yetu kwa kuwajengea Choo hiki cha Kisasa  ili kuhakikisha mtoto wa kike anawekewa mazingira rafiki anapokuwa shuleni ili aweze kuhudhuria siku za masomo kwa ukamilifu kama ilivyokuwa kwa mtoto wa kiume kwani “Ukimkomboa mtoto wa kike umekomboa Taifa zima” Ameongeza Dr. Lusako.

Aidha, amesema kuguswa kwao katika ujenzi wa Vyoo vya Mtoto wa kike imetokana na changamoto zinazoendelea kuwakabili wanafunzi kukosa vyoo bora na maji salama na safi shuleni. Tatizo hili linawaathiri watoto wa kike zaidi kwani wanashindwa kujistiri hasa wanapokuwa katika siku zao za hedhi katika mazingira ya shuleni.

Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro,ambaye pia ni afisa Taaluma Msingi,  Leah Selemani, amempongeza Mkurugenzi wa WEZESHA MABADILIKO kwa  kuwasaidia wanafunzi wa kike shuleni.

Amesema Vyoo hivyo vitapunguza utoro kwa watoto wa kike kwani wengi wamekuwa wakishindwa kufika shule wakati wa hedhi lakini baada ya ujenzi huo utasaidia sana na wanafunzi watahuduhuria shule wakiwa katika hali hiyo maana ipo sehemu salama kwao katika kujisafisha na kujilinda.

Mama Selemani , ameowaomba Wazazi kuwahimiza watoto kwenda shule mara baada ya kupata hedhi kwani mabadiliko hayo yanazuilika wakiwa shuleni.

“Dada yetu Dr. Lusako, amefanya jambo zuri sana, sisi kama Manispaa tunampongeza sana kwa jitihada zake, hii ni mbinu nzuri sana , hiki ni choo cha 3 kwa Manispaa yetu, kimoja kipo Tubuyu Sekondari, kingine kipo Kihonda Sekondari hakijaisha na mategemeo yetu kiishe mwaka huu unaokuja wa 2022, choo hiki  kitasaidia kupunguza utoro kwa watoto wa kike wanaoingia katika siku zao (hedhi), kumekuwa na changamoto wanafunzi kubeba pedi kwenye begi na kwenda nazo shule wengine wanaenda kuomba ofisini , lakini kwa hali hii ni vigumu hata kutambua mtu yupo katika hali gani maana vifaa vyote vitakuwa chooni ni yeye kwenda na kujihudumia”Amesema Mama Selemani.

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.