Header Ads

DIWANI LUJUO AAHIDI KUTATUA CHANGAMOTO ZA ELIMU KATA YA BOMA.

 

DIWANI wa Kata ya Boma Manispaa ya Morogoro,Mhe. Athuman Lujuo, (kulia) akizungumza jambo na Waalimu , pamoja na Afisa Elimu Kata katika ziara yake ya kukagua maendeleo ya shule ya Sekondari Tubuyu.


Madarasa ya UVIKO-19 Shule ya Sekondar

DIWANI wa Kata ya Boma Manispaa ya Morogoro,Mhe. Athuman Lujuo,  ameahidi kutatua changamoto za elimu zinazoikumba shule  zake zilizopo Kata ya Boma ikiwamo shule ya Sekondari Tubuyu  ambayo kuna changamoto za uchakavu wa  sakafu ya madarasa  pamoja na uchakavu wa ubao wa kufundishia.

Kauli hiyo ameitoa mapema  Desemba 17/2021 , wakati alipokua katika ziara ya siku moja ya kukagua miundombinu ya shule zilizopo Kata ya Boma  ambapo katika Shule ya Sekondari Tubuyu amekuta madarasa  manne (4) sakafu imechakaa na kuharibika na madarasa matatu (3) ubao wa kufundishia umechakaa.

Akizungumza juu ya ziara yake, Mhe. Lujuo,amesema kuwa kwa sasa jukumu kubwa ni kuhakikisha Kata ya Boma inapiga hatua katika Nyanja zote.

 “Changamoto kubwa ambazo nimeziona na tunazo katika Kata yetu ya Boma hususani katika Sekta ya elimu ni uchache wa vyumba vya madarasa, uchakavu wa sakafu na mabati, uhaba wa vifaa vya kufundishia, uchakavu wa ubaoa wa kufundishia pamoja na uahaba wa vyumba za Waalimu, katika kuona hizi changamoto zinatatuliwa , nitahakikisha changamoto zinazozikabili shule zetu zilizopo Kata yetu ya Boma ninazitatua kwa kutumia nguvu zangu binafsi kama Diwani kwani kitendo cha wananchi kunichagua kimeonesha kuwa na Imani na mimi , hivyo nina kila sababu ya kuhakikisha changamoto za shule hizi nazitatua kwa haraka kipndi hiki ambacho wanafunzi wapo likizo ili wakifungua shule wakute mazingira mazuri na arafiki kwa kusoma” Amesema Mhe. Lujuo.

Mhe. Lujuo, amesema kuwepo kwa mazingira ambayo sio rafiki shule  ni moja ya sababu ambayo inaweza kuwapelekea wanafunzi kutofanya vizuri katika masomo yao.

Katika hatua nyengine, Mhe.Lujuo, alipata nafasi ya kukagua ujenzi wa madarasa yanayojengwa chini ya moango wa UVIKO-19 katika Shule ya Sekondari Morogoro na kuridhishwa na kazi inayoendelea huku akiwataka mafundi kuafnya kazi usiku na mchana ili kukabidhi mradi huo kwa wakati.

Hata hivyo mara baada ya kuona madarasa hayo , amempongeza Rais wa Awamu ya Sita, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha za ujenzi wa madarasa hayo huku akiwataka walimu, Wazazi kuhakikisha wanashirikiana kikamilifu ili kuongeza ufaulu katika Shule hiyo.

Amesema, moja ya jukumu Kuu la Afisa elimu Kata ni  katika  ufuatiliaji wa maendeleo ya shule za msingi na sekondari za serikali pamoja na shule za watu binafsi zilizopo katika Kata ya Boma  katika kuona ubora wa taaluma unakuwa wakiwango cha juu.

Katika kuona hilo la ufaulu kwa Kata yake linafanikiwa, amemuagiza  amemugiza Afisa Elimu Kata ya Boma, kuhakikisha anafanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa  shule za Msingi na Sekondari ili mapungufu yanayobainika yaweze kufanyiwa kazi kwa wakati kwa ajili ya kuboresha taaluma shuleni na ufaulu wa wanafunzi.

Kwa upande wake, Mtendaji wa Kata ya Boma, Prisca Mawala,  amemshukuru sana, Mhe. Lujuo, kwa kwenda kuwatembea shule hizo kwani anaona ziara hiyo itazaa matunda kwa kutatua  baadhi ya changamoto zao ambazo zimekua zikizikabili shule hizo hususani shule ya Sekondari Tubuyu.


No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.