MPANJU APONGEZA WANANCHI WA KIEGEA 'A' MANISPAA YA MOROGORO KUANZA UJENZI WA KITUO CHA POLISI
NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Amon Mpanju, amewapogeza Wananchi wa Mtaa Kiegea
‘A’ Kata ya Kihonda Manispaa ya Morogoro
kwa maamuzi ya kuanza ujenzi wa Kituo cha Polisi kwa kutumia nguvu kazi za
Wananchi na michango yao.
Pongezi hizo amezitoa wakati wa ziara yake ya
kukagua maendeleo ya ujenzi huo Machi 31-2026 akiambatana na Viongozi
mbalimbali ngazi ya Mkoa wa Morogoro na Manispaa ya Morogoro.
Akizungumza na
wananchi waliojitokeza katika mapokezi hayo, Mpanju, amewahamasisha
kumalizia ujenzi wa kituo hicho kwa wakati ili kiweze kuwahudumia pamoja na
wananchi maeneo jirani ikiwemo Kata tatu Lukobe, Mkundi na Kihonda.
Aidha, Mpanju,
ametoa jumla ya mifuko 45 ya saruji, huku akiwataka wadau mbalimbali waendelee
kuchangia na wizara yake itahakikisha ujenzi huo unakamilika ifikapo Desemba
2026 na kuona ndoto ya wananchi wa Kiegea ya kuwa na Kituo cha Polisi kwa ajili
ya usalama na ulinzi wa mali zao
unakamilika.
Mpanju, mbali na kukagua ujenzi huo, pia amekuatana na makundi
mbalimbali katika Ukumbi wa Kapinga Mkundi ikiwemo Kundi la Wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu kwa ajili ya kuwaelezea fursa
zinazotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii.
Miongoni mwa fursa alizozitaja ni fursa ya mikopo ya asilimia 10
ya Wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu, fursa ya zabuni za serikali ya
asilimia 30 kwa makundi maalum , fursa ya mikopo kuendeleza wafanyabaishara
ndondogo maarufu machinga pamoja na fursa zinazotolewa na Wizara ya Maendeleo
ya Vijana ya bilioni 200 kutoka kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Naye Meya Manispaa ya Morogoro, Mhe. Khalid Matengo, amewapongeza
wananchi kwa hatua walichukua kwani usalama wa wananchi unaanza na wao wenyewe.
Matengo,amesema kuwa katikakuona ujenzi huo unafanikiwa Ofisi ya
Meya itachangia jumla ya matofali 2000 ili kuwaunga mkono wananchi wa Kiegea
kifanikisha ujenzi huo.
Kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Morogoro , Christopher Komba,
amesema Manispaa ya Morogoro katika ujenzi wa Kituo hicho umesaidia vifusi na
kutoa gari kwa ajili ya ubebaji wa vifaa lakini bado inaendelea kuona nguvu ya
kuongeza ili ujezi huo ukamilike na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.
Diwani wa Kata ya Kihonda, Eng. Mhe. Ramadhani Myolele, amesema
mradi huo umeibuliwa na wananchi mara baada ya kuona changamoto za kiuharifu na
kuanza kucnagia fedha na kutoa nguvu kazi.
Eng. Myolele ,amesema kuwa , mradi huo una malengo ya kusogeza
huduma za kipolisi karibu na Wananchi pamoja na kujenga mahusiano mazuri kati
ya Polisi na Wananchi.
Kwa upande wake, wa
Mtaa wa Kiegea ‘A’ Ezekiel Songa, amewapongeza wananchi kwa kutoa nguvu kazi na
kuchangia fedha za kuanza kwa Kituo hicho huku akisema ili Polisi wafanye kazi kwa uadilifu
wanatakiwa kuwa na mazingira bora ya kufanyia kazi, hivyo kituo hicho kitakapo
kamilika kitakuwa msaada kwa wananchi wa Mtaa wa Kiegea ‘A’ ,Kata ya Kihonda na
Kata jirani ikiwemo Lukobe, Mkundi pamoja na Katab ya Kihonda
Mkazi wa Kiegea ‘A’ Undule Anthony, amesema walikuwa
wanateseka kufuata huduma ya Polisi wanasafiri umbali mrefu kwa kutumia gharama
ya shilingi 5,000/= hivyo kumalizika kwa mradi huo kutawapunguzia gharama za
kusafiri umbali mrefu na kupunguza vitendo vya uharifu katika Mtaa wa Kiegea.
















Post a Comment