Header Ads

DC KILAKALA AWATAKA WANANCHI KUFUCHUA WAHARIFU WA VITENDO VYA UKATILI DHIDI YA WATOTO



MKUU wa Wilaya ya Morogoro Mhe.Mussa Kilakala,amewataka wananchi kuwafichua wanaotenda makosa ya ukatili dhidi ya Watoto katika  Jamii.

Kauli hiyo ameitoa Juni 16-2025 katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika Manispaa ya Morogoro iliyofanyika eneo la Uwanja wa Mpira wa Miguu Shule ya Msingi Mwembesongo.

Akizungumza na wananchi waliojitokeza katika maadhimisho hayo,DC Kilakala,amesema siku ya Mtoto wa Afrika ni vyema jamii ikafanya tathimini ya hali halisi iliyopo kwa kutafakari Kauli mbiu ya Siku ya Mtoto wa Afrika mwaka 2025 inayokumbusha kuangalia mienendo dkatika makuzi na malezi ya Watoto wakiwa nyumbani, nje ya nyumbani kwa kuangalia walipotoka,walipo na wanapoenda na kurekebisha mapungufu ili kuangalia kesho yao kwa malezi bora.

ameiomba Jamii kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kuhakikisha vitendo vya ukatili dhidi ya Watoto vinakemewa vikali na kuzuiwa katika Jamii.

DC Kilakala, amewataka wazazi/walezi  na wadau wa masuala ya Watoto kwa kila mmoja aone kwamba ana wajibu wa kuleta mabadiliko chanya kwa jamii kushiriki kikamilifu katika kulinda na kutekeleza kwa vitendo Haki za Watoto.

“Tuna wajibu wa kutoa elimu kwa Watoto wetu juu ya mabadiliko mbalimbali ya kijamii ikiwemo matumizi ya teknolojia ambapo ukuaji wake uendane na ukuaji wa elimu ili matumizi yake yasiwe na athari hasi katika maendeleo ya ukuaji na hatma ya Maisha ya watoto wetu” Amesema DC Kilakala.

Mwisho,ameitaka Jamii kukabiliana na mmomonyoko wa maadili kwa kukemea hali ya ukiukwaji wa maadili mema hususani katika kuingiza mila,desturi na tamaduni zisizokubalika na kulinda mila  na desturi nzuri kwa Watoto na jamii kwa ujumla.

Naye Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Morogoro,Faraja Maduhu,amesema siku hii huadhimishwa kwa lengo la kutambua thamani,utu na umuhimu wa Mtoto Duniani kutokana na mauaji ya Watoto takribani 2000 yaliyofanywa na utawala wa Makaburu katika Kitongoji cha Soweto Nchini Afrika Kusini tarehe 16,Juni mwaka 1976.

Maduhu amesema Kauli Mbiu yam waka 2025 inaitaka Jamii kutafakari upatikanaji wa haki haki za Watoto tangu zilipoanzishwa na Sera ya Maendeleo ya Mtoto yam waka 2008 ambayo inakumbusha wazazi au walezi na jamii haki tano za msingi za mtoto ikiwemo kuishi, kulindwa, kuendelezwa,kutobaguliwa na haki ya kushiriki na kutoa maoni kwa mambo yanayomuhusu.

Kwa upande wa Mratibu wa Dawati la Maendeleo ya Mtoto Manispaa ya Morogoro,Joyce Mugambi,amesema elimu za kupinga ukatili ulitolewa kwa Kata 12 na kufikia shule za Msingi 14 na vituo vya kulelea Watoto 4 ,kutoa elimu Kamati za usalama shuleni kwa Zaidi ya shule za Msingi 128,kuhuisha Mabaraza ya Kata 23 na Mitaa 135 ,kutoa elimu juu ya haki na wajibu ambapo jumla ya shule 17 za Msingi na wanafunzi Zaidi ya 658 wamefikiwa na elimu hiyo.

Kauli Mbiu ya Siku ya Mtoto wa Afrika mwaka 2025 inasema “Haki za Mtoto:Tulipotoka,Tulipo na Tuendako”. 

No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.