Header Ads

AFISA TARAFA MANISPAA YA MOROGORO ATAKA MAPAMBANO DHIDI YA UDUMAVU.

Afisa Tarafa Manispaa ya Morogoro, Winfred Kipako, akizungumza na wananchi waliohudhuria katika Siku ya Lishe na Afya Kata ya Mwembesongo.
Mtendaji wa Kata ya Mwembesongo, Amina Said, akizungumza  na wananchi waliohudhuria katika Siku ya Lishe na Afya Kata ya Mwembesongo.
Mtendaji wa Kata ya Mwembesongo, Amina Said (wapili kulia) ,akizungumza na wataalamu wa Lishe na Afya kutoka Chuo Kikuu cha SUA.

 AFISA Tarafa Manispaa ya Morogoro, Winfred Kipako,  ametaka   wadau wa lishe   kupambana  kutokomeza udumavu ndani ya Manispaa ya Morogoro hususani wakazi wa Kata ya Mwembesongo  ili  kuwa na jamii  bora  isiyo na udumavu .

Kauli hiyo ameitoa leo Agosti 28/2021 katika uzinduzi wa Siku ya Lishe na Afya  Kata ya Mwembesongo, iliyofanyika katika eneo la Ofisi ya Kata.

Akizungumza  na Wananchi waliohudhuria katika siku hiyo ya Lishe , Kipako, amesema kuwa Manispaa ya Morogoro ni miongoni mwa Manispaa ambazo hazina shida ya vyakula, hivyo  si sahihi Kata ya Mwembesongo, ikawa  na tatizo la udumavu  wakati  chakula kipo  cha kutosha .

"Kwanini  Mwembesongo   tuendelee   kuwa na uduamavu  wakati tunalima matunda ya kutosha  ,tuna wanga wa  kutosha na mboga za majani  za  kutosha  tuna kila aina  ya  virutubisho  vya  mwili  tumekuwa na changamoto  ndogo ndogo  ambazo  zilikiukwa  toka zamani  ila sasa  ni wakati mzuri  wa  kuzifanyia kazi changamoto  hizo " Amesema Kipako.

Aidha, amesema  moja kati ya   changamoto  kubwa  ya baadhi ya  wazazi  kutozingatia  utunzaji mzuri wa  watoto  wakati  wakiwa na ujauzito  na baada ya  ujauzito   kwa kushindwa   kulea watoto  kwa  kipindi cha siku  1000  kama    inavyotakiwa  kwa  mtoto kutunzwa.
 
Kipako, amesema  kuwa suala  lishe  limekuwa na  tatizo mtambuka  katika  Taifa ,  hivyo  ni  wajibu   kwa wadau  wote  ndani ya Kata ya Mwembesongo kupambana na suala  la  lishe .

Kuwa  taifa   linapokuwa na  watu  wengi  wenye udumavu ni hatari  sana kwa Taifa  linakosa   watenda kazi  wazuri  hivyo ni lazima   kujipanga  kuona suala la  lishe  linapewa  kipaumbele kama  njia ya  kuondokana kabisa na changamoto ya  lishe  na udumavu  ndani ya  Kilakawilaya .

Hata hivyo, amesema   hali ya  lishe  inapaswa   kuongezwa   zaidi ili  kuona jamii  inatumia  vema  vyakula vinavyo zalishwa  katika  Manispaa ya Morogoro hiyo  kama  sehemu  ya kuongeza  lishe  bora kwa  jamii .

Naye Mtendaji wa Kata ya Mwembesongo, Amina Said, amesema kuwa sababu kubwa inazosababisha hali hiyo ni kutowekeza muda wa kuwa na watoto kuwalisha ipasavyo ikiwepo kuwapa pombe kwa baadhi ya maeneo, lishe duni kutokana na wananchi kutokuwa na elimu ya ulaji wa chakula cha kutosha na chenye mchanganyiko wa viini lishe.

Amina amesema , kuwa  kuwa kutokana na changamoto hiyo, Kata ya Mwembesongo, inatarajia kuweka  mikakati mbalimbali katika kuweza kupambana na hali ya utapiamlo na udumavu kwa watoto wenye chini ya miaka mitano ikiwemo kutoa elimu ya nadharia na vitendo kwa jamii kuhakikisha kwamba ulaji wa kiwango cha juu cha virutubishi unafanyika na kuzingatia unyonyeshaji katika siku 1,000 za mtoto unafuatwa.

Naye Mwananchi wa Kata hiyo, Juma Abdallah, ameupongeza Uongozi wa Kata ya Mwembesongo, kwa kuifanya Siku hiyo katika Kata hiyo.

"Tunampongeza Mgeni rasmi kwa kuacha majukumu yake na kujumuika na sisi kwa kweli leo tumepata elimu kubwa ambayo  hatukuwa nayo tunaomba elimu hii isiishie hapa bali ifike kwa wananchi zaidi ili kila mtu anufaike " Amesema Abdallah.


No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.