DC KILAKALA AWATAKA WASHIRIKI MAFUNZO UFUGAJI KUKU WA NYAMA BILA DAWA KUSAMBAZA TEKNOLOJIA HIYO KWA WANANCHI KUPUNGUZA USUGU WA VIMELEA VYA MAGONJWA KWA BINADAMU.


MKUU wa Wilaya ya Morogoro,Mhe. Mussa Kilakala,amewataka wafugaji wa kuku bila kutumia dawa kusambaza teknolojia hiyo kwa wananchi wa Wilaya ya Morogoro ili kuepusha Usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya Dawa ,UVIDA au (AMR).
Hayo,ameyasema
katika Mahafali ya kwanza ya wafugaji washiriki wa shamba darasa la ufugaji bora wa kuku wa nyama bila bila Dawa katika eneo la
Polister Klabu Machi 21-2025 ambapo kuku hao wanakuwa ndani ya wiki 5 sawa na
siku 35
“Tunataka mradi huu usambae Wilaya nzima, tutakaa Pamoja na
wafugaji , Kila mmoja atakuwa na wanafunzi wake atakaowanufaisha maarifa ambayo
FAO imempatia, hivyo mradi utawafikia watu wengi zaidi ya wanufaika wa moja kwa
moja.”Amesema DC KIlakala.
Aidha,DC Kilakala,ameishukuru Serikali chini ya Dkt.Samia
Suluhu Hassan,kwa kuwekeza nguvu katika mradi huo na kuwafanya wafugaji
kujifunza ufugaji wa kuku hao bila malipo.
Meya
Manispaa ya Morogoro,Mhe.Pascal Kihanga, amewataka wafugaji hao kukaa kikao cha pamoja kusaidia teknolojia hiyo ya ufugaji ienee kwa Kata zote za
Manispaa ya Morogoro.
Mhe. Kihanga, amesema FAO ,wamewarahisishia kupata vikundi vya mikopo vyenye
sifa ya kukopesheka kutokana na walivyojiandaa.
“Tunawashukuru
FAO, wameturahisishia vikundi vyetu kukopesheka kwa urahisi,hawa watu katika
mikopo tunawapa vipaumbele kwa kuwa wameonesha kuna kitu wanafanya “ Amesema
Kihanga.
Kuhusu changamoto ya upatikanaji wa maeneo ya ufugaji,Mhe. Kihanga ,amesema kuwa Manispaa ina maeneo makubwa hivyo vikundi vijipange watapatiwa maeneo rafiki kwa ajili ya ufugaji.
Kwa upande wa Mratibu wa Mradi wa ufugaji kuku bila kutumia dawa kutoka FAO nchini Tanzania, Dkt.Elibariki Mwakapeje,amesema ufugaji huo unahusisha kinga zaidi kuepusha kuku kuambukizwa magonjwa kwa kuzingatia usafi na kutumia vifaa kinga, lengo ni kuepusha Usugu wa , Vimelea vya magonjwa dhidi ya Dawa, UVIDA au (AMR) kwa lugha ya kiingereza.
Dkt.Elibariki,amesema Mradi unatekelezwa kwa
ushirikiano na Wizara ya Mifugo na Uvivu kwenye taifa hilo la Afrika Mashariki
ambapo utekelezaji wake unafanyika mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam na
Arusha.
Naye ,Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Manispaa ya Morogoro, Dkt. Tito Kagize,amesema Idara yao wataendelea kutoa ushirikiano mkubwa kwa wafugaji hao ili waweze kutimiza malengo yao.
Post a Comment