Header Ads

VIONGOZI WATEULE BAKWATA WAASWA KUZINGATIA UTENDAJI WA KAZI


SHEIKH Mkuu wa Mkoa wa Morogoro. Amewataka viongozi wateule kuzingatia utendaji wa kazi kwa kutumikia kazi za kidini.

Hayo ameyasema Sheikh wa Mkoa wa Morogoro ,Twaha Swalehe Kilango, katika uchaguzi wa Viongozi wa Bakwata Mkoa wa Morogoro uliofanyika Agosti.. katika ukumbi wa Mikutano wa Manispaa ya Morogoro.

Aidha, Sheikh Kilango, amewasisitizia viongozi hao wateule kufanya kazi kwa kuzingatia sheria,kanuni na Katiba ya Baraza Kuu la Waisalmu Tanzania (BAKWATA)

“Mmechaguliwa leo,mmepewa Imani kubwa ,nendeni kafanyeni kazi kwa misingi ya Katiba ya BAKWATA , ili kila mmoja akasimame kwenye nafasi yake ya utendaji kuanzia viongozi wa Wilaya na Mkoa, kazi za dini ni za kujitolea  ” Amesema Sheikh Kilango.

Aidha,amewataka viongozi hao kuacha kujifungia katika Ofisi badala yake wawafikie watu wao ili kujua changamoto zinazowakabili na kuzifanyia kazi ili iwe sehemu ya kutengeneza muunganiko mzuri wa daraja baina ya Viongozi na wale wanaowaongoza.

Hata hivyo, amewapongeza Viongozi mbalimbali kwa uvumilivu wa kujitoa kwao katika mchakato wa uchaguzi ambao umechukua muda mrefu huku akisema subira ni jambo la msingi katika kuyafikia malengo.

Mwisho,amewataka viongozi wote waliothubutu kugombea na kura hazikutosha watendelea kushirikiana nao kwa ajili ya kujenga BAKWATA na wasikate tamaa kwani uongozi ni kupokezana vijiti bado nafasi zao za uongozi zipo katika nyakati zijazo.

Miongoni mwa nafasi zilizogombewa ni Mwenyekiti wa Halmashauri Mkoa wa Morogoro , Baraza la Masheikh Mkoa wa Morogoro, Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa , Wajumbe wa Halmashauri Mkoa huku upande wa JUWAKITA nafasi zilizogombaniwa ni Mwenyekiti wa JUWAKITA Mkoa wa Morogoro, Wajumbe wa Halmashauri Kuu Taifa na Wajumbe wa Kamati ya JUWAKITA Mkoa wa Morogoro.


No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.