Header Ads

BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA MOROGORO LAADHIMIA KUUNDA KAMATI YA UFUATILIAJI WA DENI LA STENDI YA MSAMVU

 


BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA MOROGORO LAADHIMIA KUUNDA KAMATI YA UFUATILIAJI WA DENI LA STENDI YA MSAMVU

BARAZA la Madiwani Manispaa ya Morogoro limeadhimia kuunda kamati maalum ambayo itakuwa na jukumu la kwenda Ofisi ya Rais Tamisemi kukutana na Waziri wa Tamisemi Mh. Mohamed Mchengerwa ili kuona namna ya kujadili deni la shilingi Bilioni 20 linaloikabili Manispaa hiyo kutokana na ujenzi wa Stendi ya Mabasi Msamvu.

Hayo yamejiri Aprili 30-2025 katika Mkutano wa kawaida wa Baraza la Madiwani lililofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Manispaa ya Morogoro.

“Mkurugenzi amepokea barua kutoka Ofisi ya Tamisemi  ikimtaka Manispaa kulipa deni la Bilioni 20 la ujenzi wa Stendi ya Msamvu , baada ya kupokea barua  la Baraza la Madiwani tumeadhimia kuunda kamati ili tukutane na  viongozi wetu watusaidie kupata kibali cha kukutana naWaziri wa Tamisemi,  ili kuketi pamoja kuona namna ya deni hilo linalipwaje, Rais wetu ni msikivu sana, tunaimani kubwa katika mazungumzo yetu hili deni atatusaidia kwani deni hilo sio la viongozi bali ni deni la wananchi wote wa Manispaa ya Morogoro ambapo tutalazimika kuacha maendeleo mengine kulipa deni hili kupitia fedha za mapato ya ndani” Amesema Meya Kihanga.

Naye Diwani wa Kata ya Kihonda, Mhe. Hamisi Kilongo,amesema wananchi wa Manispaa ya Morogoro wana tunaomba  Rais Dkt. Samia aone namna ya kutusaidia kwani Morogoro imekuwa kinara wa kuongoza kwa kura za Rais , hivyo deni ambalo lipo mbele ni kubwa na linaweza kutukwamisha  shughuli nyingi za maendeleo.

“ Tunaimani na Rais wetu,amefanya makubwa sana kwenye Mkoa wetu wa Morogoro hususani Manispaa ya Morogoro,tumepokea fedha nyingi za miradi ya maendeleo,kwa hili la deni la Bilioni 20,tunamuomba sana Mhe. Rais alisimamie vyema, kwani bado mapato yetu ni madogo,tukilipa deni itafanya maendeleo ya Manispaa kusimama”Amesema Mhe. Kilongo.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Mafiga Mhe. Thomas Butabile, amesema Dkt Samia amejenga Stendi bora za kisasa, na amekuwa mstari wa mbele katika kuwaletea maendeleo wananchi,hivyo ameomba kuwafikiria zaidi Manispaa juu ya deni hilo ambalo ni mzigo mkubwa kwani bajeti ya Manispaa haijitoshelezi na hata zile ndoto za kuwa Jiji zitakuwa zimegonga mwamba.

 

Ikumbukwe kwamba Ujenzi wa Stendi ya Msmavu, umekuja kufuatia Manispaa ya Morogoro kwa kushirikiana na Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF)  kuunda  Kampuni ya ubia iliyojulikana kama Msamvu Properties Company (T) Limited ambayo ilikuwa na jukumu la kusimamia shughuli zote za stendi ikiwa ni pamoja na ukusanyaji wa ushuru wa stendi, ujenzi na uendeshaji wa miradi yote itakayokuwa inatekelezwa na Kampuni kwa niaba ya taasisi hizo mbili.

 


No comments

Theme images by A330Pilot. Powered by Blogger.